Sunday, February 17, 2013

UTENZI WA KATIBA 601-799


601.
Bila hivyo hufulia,
Mengi yakawakimbia,
Na nchi kujikondea,
Minofu ikififia.
602.
Mawasiliano twajua,
Watu yanasaidia,
Na kilichobakia,
Unyonyaji kupungua.
607.
Fedha zikichukuliwa,
Na wachache walokuwa,
kawaida inakuwa,
Ni vibaya kutumiwa.
608.
Vocha bei kupungua,
Na muda kuongezewa,
kiasi kitabakia,
Mengine kujifanyia.

609.
Dijito teknolojia,
Jinsi ninavyoelewa,
Urahisi yatakiwa,
Maisha kutufanyia.
610.
Ujanja ukipungua,
Gharama haitakuwa,
Mbadala kujaliwa,
Kawaida kurejea.

611.
Ila tukiwaachia,
Wajanja waliokuwa,
Pasina kuwa sheria,
Hili kuliangalia.
612.
Kwa miaka kama mia,
Mlaji kumrarua,
Hii ndiyo dunia,
Mabepari twawajua.
613.
Kompyuta Tanzania,
Budi kujitengezea,
Zetu zilizokuwa,
Kiswahili zatumia.
614.
Ni lugha iliyokuwa,
Kila mtu atumia,
Mwanzo wameanzia,
Wenye simu twasifia.
615.
Sasa ni kufatia,
Kompyuta kutumia,
Na mtandao ukawa,
Kiswahili kidedea!
616.
Vizuri tukijitoa,
Vyuo tutavifungua,
Kwa tovuti kutumia,
Afrika kuenea.
617.
Na ajira zikajaa,
Afika kufunzia,
Kiswahili kikakua,
Na uchumi kuinua.
618.
Nacho tusichojaliwa,
Viongozi wakujua,
Njia wanaotambua,
Wapi pa kuelekea.
619.
Vijiji kubwa hazina,
Kuvitunza vikafana,
Tena pasina hiyana,
Kwani tumevionea.

620.
Huduma nyingi zavia,
Kila mtu anajua,
Muongo unatakiwa,
Haya tuawapatia.
621.
Maji kutiririka,
Vijijini tunataka,
Waache kuhangaika,
Kinamama kuadhirika.
622.
Umeme kutochelewa,
Nyuma ukayafatia,
Gizani hatukuumbiwa,
Ni nani asiyejua.
623.
Nyumba nimeongelea,
Zastahili familia,
Kwa mbinu kujengewa,
Na ajira zikatoa.
624.
Hayo yakishakuwa,
Ndege yetu itapaa,
Mengine kuangalia,
Hali bora kufikia.
625.
Takwimu za Tanzania,
Watu shaka watilia,
Katiba ingetwakiwa,
Na hili kuliondoa.
626.
Ninachofikiria,
Mamlaka kuundiwa,
Na mtu isoingiliwa,
Kazi ikajifanzia.
627.
Kwa hivyo kuaminiwa,
Uhuru ikishajaliwa,
Jukumu ikalipewa,
Ukweli kupigania.
628.
Uongo kukaataa,
Na waongo kuumbua,
Mkuu hadhi akawa,
Katiba kumwangalia.
629.
Ya vyama yasiyofaa,
Hayo tutayaambaa,
Na ikulu ya kuzua,
Ukweli tukaujua.

630.
Ya tume yenye hadaa,
Yote tukayafichua,
Sensa bora kujaliwa,
Muongo kat ukiwa.
631.
Dawa tungejitambua,
Mbali tungeishakua,
Uizi uliingia,
Hakuna wa kuaminiwa.
632.
Katiba inatakiwa,
Wa jadi kuangalia,
Na msaada kupewa,
Vyao wakajiundia.
633.
Za asili tungetoa,
Na za kisasa kuzua,
Kama Wachina tukawa,
Uchumi tukajaliwa.
634.
Hakika hapa twapwaya,
Ila cha babu kikiwa,
Sasa kinachosahauliwa,
Na kingine kungojewa.
635.
Mavazi hatujaamua,
Na miaka yaishia,
Ni sanaa imekuwa,
Ndee-nani ayajua!
636.
Inacheka historia,
Kigugumizi kikiwa,
Wapi tulipopotea,
Ila usanii kuvaa?
637.
Thamani inatakiwa,
Ya mzawa Tanzania,
Vipi Mwadui akawa,
Sawa na kusikokuwa.

638.
Na thamani ni uchumi,
Ardhini uliokuwa,
Huo ukichanganuliwa,
Mwananchi akapewa.
639.
Ya Wazungu na Asia,
Mabwana wakaja kuwa,
Hapo wasingefikia,
Na thamani tungekuwa.
640.
Saluti tungepigiwa,
Kama kwa wenye kujua,
Waarabu maridhia,
Sana wanaheshimiwa.
641.
Qatar ukiingia,
Na Dubai nako pia,
Hili utaligundua,
Wivu ukakuingia.
642.
Imeshazuka tabia,
Wakubwa kujifanzia,
Bila sisi kuyajua,
Na kisha kudharauliwa.
643.
Na kisha kudahauliwa,
Na matusi kutupiwa,
Hili ninawaambia,
Kubaya twaelekea.
644.
Mtu hauwezi kuwa,
Pasina na watu kuwa,
Ukitaka  kulijua,
Porini ukitupiwa.
645.
Wakubwa mngerejea,
Nafsi kuziangalia,
Ukubwa sio kupaa,
Au malaika kuwa.
646.
Ni watu wa kujijua,
Ndio nchi hujaliwa,
Ila wasiojitambua,
Kwao nchi huangamia.

647.
Mtakatifu hujawa,
Hadi unapojifia,
Ulimi ukiamua,
Unaweza kuchafua.
648.
Unaweza kuchafua,
Na motoni kwenda kaa,
Mazuri uliyodhania,
Yote yakawa kinyaa.
649.
Ni chafu historia,
Ya nchi hii Tanzania,
Ushiriki ni tanzia,
Kuzikwa ulishajifia.
650.
Mchezo wakichezewa,
Enzi zilotangulia,
Pahala wakaishia,
Vijiji vikawa baa!
651.
Kinyume kiangalia,
Yahudi wametimia,
Vyao wamevinyanyua,
Kitega uchumi kuwa.
652.
Sisi tuliochezea,
Shilingi tukaachia,
Chooni ikaingia,
Twawa ni wa kufulia.
653.
Tulichokikosea,
Raia tulihadaa,
Kwa king'enge kwishia:
'Manipulation' hatua.
654.
Tiba hatukuijua,
Therapy kufafanuliwa,
Tukaganga yetu nia,
Na nyufa kuzitumia.
655.
Taarifa nayo pia,
Hiyo hatukuifikia,
Kwani tulipoishia,
Hatujui ni 'Informing'.

656.
Leo ukitembelea,
Vijiji vya Tanzania,
Ufahamu wafulia,
Ila tu yao kujua.
657.
Kwao ni giza dunia,
Mawasiiano sanaa,
Kwa simu isipokuwa,
Na mnara palokuwa.
658.
Yao wakaongelea,
Na umbeya kuupokea,
Ila habari kujua,
Bado wanatahiniwa.
659.
Ushauri umevia,
Nani watakusikia,
Imeshazuka tabia,
Kila kitu wanajua.
660.
Wazo ukiwaachia,
Haraka watakuibia,
Mkia wakauchukua,
kishwa wakakuachia.
661.
Nusunusu huyazua,
Ndio kufa kuwa kawa,
Nam sintosikitikia,
Pasi katiba kuwa dawa.
662.
Kwingine tukachagua,
Kwenda kuchangamkia,
Kura tukajiombea,
Ndiko kulikoendelea.
663.
Na mtu wasiyekuwa,
Au uoga kwingia,
Nyuma tukishabakia,
Huko si kuendelea.
664.
Hatua zinazotakiwa,
Ni ubia kuingia,
Pamoja wakayazua,
Nchi yatayonyanyua.

665.
Hapo wakishafikia,
Mamlaka kukaimiwa,
Huru ikiwa mikoa,
kasi yetu ya kupaa.
666.
Ushindani ukiingia,
Wa kweli uliokuwa,
Wavivu watajijua,
Wenyewe kujiondoa.
667.
Wabebwa  watang'aamua,
Ngazi wakaziachia,
Barubaru wakatwaa,
Kilele kuelekea.
668.
Imekua Tanzania,
Nje budi kuingia,
Biashara kuzizua,
Na kampuni kwanzisha.
669.
Bakhresa kawa ni taa,
Njia anazipasua,
Wivu kutokumuonea,
Ila tuwe twamsaidia.
670.
CRFB wapaa,
Burundi weshaingia,
Afrika kuenea,
Pengine waazimia.
671.
Katiba ikichochea,
Kupanuka tasnia,
Makampuni Tanzania,
Kimataifa yakawa.
672.
Hilo jema lingekuwa,
Na chati kutunyanyua,
Watoto kuajirriwa,
Nchi za nje kukaa.
673.
Lugha watajisomea,
Zitawalazo dunia,
Kizulu wakakijua,
Sambamba nacho Kichina.
674.
Kihausa kukijua,
Na Kiarabu nacho pia,
Kazi wakajifanzia,
Zing'arishazo Tanzania.
675.
Hatua itafikiwa,
Umma upate chipua,
Mamlaka kuyagawa,
Washike Watanzania.
676.
Hapo watakaobakia,
Si rushwa waliotoa,
Ila wanaojijua,
Na wajibu kutimia.
677.
Umaskini uchafu,
Unayo mbaya harufu,
Hili kujitaarifu,
Wote tukalikataa.
678.
Kuna wanaotumia,
Kuyapata manufaa,
Hao ni kuwashushua,
Akili zikarejea.
679.
Ziengwe rasilimali,
Kutufaa bilkuli,
Sasa kwa ilivyo hali,
Ufisadi umejaa.
680.
Juu walojikweza,
Wataka kuzimaliza,
Wawa kama waigiza,
Ila wanatuchuuza.
681.
Mikataba waridhia,
Kama vile ya kijuha,
Au wananunuliwa,
Psina sisi kujua.
682.
Sasa kinachotakiwa,
Tamko leltu kutoa,
Rasilimali ni dia,
Tunazimiliki raia.

683.
Pale kwetu tukivua,
Hiyo ni yetu ngekewa,
Mola katubarikia,
Japo hatukulijua.
684.
Iwepo asilimia,
Daima ya kuachiwa,
Kisha ndiyo kugaiwa,
Kitaifa Tanzania.
685.
Thamani kuichungua,
Iwe ni yetu tabia,
Na huo mtaji ukawa,
Kwa wazawa walokuwa.
686.
Waweza kujiuzia,
Au hisa kuridhia,
Umiliki wakajua,
Hali wanajinyanyua.
687.
Kijiji kikiamua,
Ubia kitawania,
Yao wakajifanyia,
Kisha wakajichomoa.
688.
kubwa wanayofanza,
Imani wanaikwaza,
Twaona wanajikweza,
Pekee  wakajaliwa.
689.
Wao wakishapatiwa,
Sisti  husahauliwa,
Mshirika wao kuwa,
Mwekezaji Tanzania.
690.
Tunaona wanapwaya,
Urahisi wanajitia,
Kidogo wanachochukua,
Mbona twaweza chimbua?
691.
Wanatakiwa kukua,
Njaa kuacha ugua,
Ili wapate tambua,
Ufakiri si laana.

692.
Wote tukijigawia,
Wala hautapungua,
Na kichowazuzua,
Kaburi wakimbilia.
693.
Yatayokujakutokea,
Mazuri hayatakuwa,
Salama hapatakuwa,
Ila maisha kuvia.
694.
Vipaji vya tasnia,
Katiba inatakiwa,
Muongozo kuutoa,
Kwa haki vikalelewa.
695.
Sasa yanayotokea,
Mmoja mmoja kuwa,
Mwenyewe akiamua,
Nani kumsaidia.
696.
Mifumo kuandaliwa,
Wote wakashughulikiwa,
Na zikawepo sheria,
Hili kuliangalia.
697.
Watoto wa Tanzania,
Haki sawa watakiwa,
Pasiwe kupendelea,
Na wengine kuonewa.
698.
Vijana wa Tanzania,
Fursa sawa kupewa,
Sio kwa vitendo na nia,
Ila kwa kazi kufanziwa.
699.
Wazee wanatakiwa,
Baraza wakaundiwa,
Wala sio kutumiwa,
Kama vile kitambaa.
700.
Kama vile kitambaa,
Mikono kujifutia,
Ila wakatunukiwa,
Nchi kuizungumzia.

701.
Nchi kuizungmzia,
Pasina kuegemea,
Na kama ni kuamua,
Haki ikawatangulia.
702.
Yao pia kwangalia,
Nafuu kujipatia,
Leo wasahauiwa,
kila mtu anajua.
703.
Twaweza kuwafufua,
Mchango bora kutoa,
Nchi ikatengamaa,
Na imara kwenda kuwa.
704.
Wazee wamejaliwa,
Umri walioukaa,
Maisha wanayajua,
Na vituko kung'amua.
705.
Wasipokuwa na njaa,
Huingia  ushujaa,
Udhia wakakataa,
Halali kupigania.
706.
Ndivyo inavyotakiwa,
Mchango bora kutoa,
Nchi ikaendelea,
Kwa aali nadharia.
707.
Kinamama Tanzania,,
Makubwa wangetufanyia,
Wenyewe wangejijua,
Wala sio kutumiwa.
708.
Taasisi yatakiwa,
Kufunzwa sosholojia,
Pia na saikolojia,
Waweze kujikomboa.
709.
Kisha wakaongezewa,
Uongozi kuujua,
Na fitina wakatoa,
Wenyewe kujipendelea.
710.
Wajanja wakizaliwa,
Watu hutaka nunua,
Bei wakajipangia,
Ili yao kutimia.
711.
Husahau yakujua,
Hadi wakaulizia,
Hususan inapokuwa,
Magogo wanawekewa.
712.
Upande wanaujua,
Sana uliolegea,
Hukohuko huingia,
Vibeti kuvibetua.
713.
Sasa nchi yatakiwa,
Wananchi kuamua,
Si kugeuzwa majuha,
Mambo wakalazimishwa.
714.
Vikundi kuzinduliwa,
Jamii ikavitumia,
Yao kuyapigania,
Pasina kuingiliwa.
715.
Mgao ukitokea,
Watu wanaonunua,
Na wanaokataa,
Wao kutonunuliwa.
716.
Kuuzwa wanaokataa,
Sauti pia kusikiwa,
Sio tu mkawafaa,
Wanaotaka nunua.
717.
Ustawi wa jamii,
Kama hai silijui,
Naona haina uhai,
Kwa yanayoendelea.
718.
Juhudi zinatakiwa,
Idara kuiangalia,
Hapo ilipotiwa,
Naona inazidiwa.

719.
Idara ingelikuwa,
Mamlaka Tanzania,
Kaziye kuangalia,
Wanyonge waliokuwa.
720.
Kinamama walofiwa,
Na waume nao pia,
Mayatima Tanzania,
Uyatima wakomaa.
721.
Nani wa kuwaangalia,
Ila wa kuwahurumia,
Katika inatakiwa,
Hili likatatuliwa.
722.
Tunazo rasilimali,
Zinaosha kulhali,
Kushindwa uanzali,
Au utu watuishia.
723.
Hili pia laendana,
Na wa mitaani wana,
Walikuwa wachache jana,
Hivi leo ni mamia.
724.
Tutakuja pata laana,
Hili tusipolisana,
Yetu tukaharibiana,
Kwa hawa kuwaambaa.
725.
Watakuja changanyikana,
Wakashidnwa elewana,
Hepu wakaanza pambana,
Dhiki zikawanukia.
726.
Mifumo tumeishiwa,
Wala wengi hawajawa,
Ari tungelijaliwa,
Haya yasingetokea.
727.
Vijana twawaachia,
Paka tukawatishia,
Hofu zikiwaishia,
Tuna letu nawambia.

728.
Sasa kinachotakiwa,
Ni miundo kuzindua,
Na mifumo kufumua,
Upya tukajishonea.
729.
Hatuwezi tukalia,
Ajira zinapotea,
Na matatizo twajua,
Kedekese yamejaa.
730.
Matatizo Tanzania,
Fursa yaweza kuwa,
Vijana wakielewa,
Ajira kwao ikawa.
731.
Nyumba hatujajaliwa,
Na kiasi zapugnua,
Vijijini ni balaa,
Si nyumba viota  huwa.
732.
Viwanda tukianzia,
Mbali mbali vyatakiwa,
Si wote moja kuzaa,,
Uzalshaji kugawa.
732.
Mikoa kuchaguliwa,
Viwanda -mbao kuwa,
Ubora wakishakuwa,
Dunia kuwanunua.
733.
Vya vyuma vinatakiwa,
Mali ghafi kuzitoa,
Wengine wakanunua,
Yao kujitengezea.
734.
Na vyakula navyo pia,
Viwanda vyake vyafaa,
Pahala tukachagua,
Rahisi panapokuwa.
735.
Aidha vinywaji pia,
Mikoa tungechagua,
Hyo ikatuzalishia,
Tusambaze TanZania.

736.
Saruji nayo mbolea,
Hivyo hivyo kuvigawa,
Pamoja vinapokaa,
Gharama zinapungua.
737.
Kilimo tukiamua,
Kitaajiri mamia,
Mtadi tukijitoa,
Kimasomaso ikawa.
738.
Msingi wakipatiwa,
Na chakula kugawia,
Wapo wataoridhia,
Kwenda kujitegemea.
Na uvuvi nako pia,
idha na kujifugia,
Na viwanda kuvizua,
Vya msingi kuzalisha.
739.
Vijijini nawambia,
Kwingine kwanistua,
Milioni wakipewa,
Wanaweza kujitoa.
740.
Wanaweza kujitoa,
Uongozi wakipewa,
Haya unayoyajua,
Njia ukawaonyesha.
741.
Taasisi zimezuka,
Huko hazijawahi fika,
Elfu kumi zinataka,
Zikaweza kukomboa.

742.
Benki kuu ikitaka,
Mayai inayoweka,
Ikatamia hakika,
Nchi juu itapaa.
Pesa kidogo ni dawa,
Mtizo kuondoa,
Masikini walokuwa,
Utajiri kunukia.
743.
Labda upo mwongozo,
Ulifanyalo mzozo,
Waogopa wenye nazo,
Umaskini ukiisha?
744.
Minong'ono yajaa,
Mtaji uliozuliwa,
Ni umasikini kulea,
Kutawala Tanzania.
745.
Makabila Tanzania,
Urithi tulojaliwa,
Uhaini kuyaua,
Kwa lolote lilokuwa.
746.
Umoja tumejaliwa,
Twajivuna Tanzania,
Na kitakachoundoa,
Ufisadi si kabila.
747.
Matabaka yataua,
Si ukabila wa lugha,
Umoja tuliouzua,
Mbali wakajitupia.
748.
Rushwa itauondoa,
Si makabila Tanzania,
Kwa jinsi inavyoenea,
Na watu kuivumilia.
749.
Makabila kuenziwa,
Iwe ni yetu tabia,
Makumbusho yakapewa,
Kuhifadhi historia.
750.
Na kwayo teknolojia,
Lugha zikahifadhiwa,
Nani anayeyajua,
Mbele vitatusadiia?
751.
Kawaida ni sheria,
Kwa watu wasiojua,
Udini ukitumiwa,
Hili kuondoa baa!
752.
Wapo wanaojizuzua,
Kawaida kuiua,
Budi kushughulikiwa,
Ndiyo haki ilokuwa.
753.
Mapya tukillia,
Na vitisho kutmia,
Wajinga waliokuwa,
Wataona wasikiwa.
754.
Watazidi  kuroroma,
Na kuzizusha nakama.
Pakawepo uhasama,
Wa kijinga Tanzania.
755.
Mfano hili la kuchinja,
Wajua kina Masanja,
Dini moja walichinja,
Na wote tukaridhia.
756.
Ugumu halijakuwa,
Kuliko vita kuzua,
Serikali kuamua,
Kafiri kuruhusiwa.
757.
Ila tangazo kutoa,
Hakuchinjwa kauiwa,
Mnyama aliyekuwa,
Si halali kununua.
758.
Mabucha tukayatenga,
Yao yakatabandanga,
Na halali kuyakinga,
Yasije kuchafuliwa.
759.
Kuna wana Tanzania,
Wembe sasa walilia,
Kwa moja kuligundua,
Wadhani yote wajua.
760.
Kazi tukijipangia,
Na ufanisi zikawa,
Ufanifu nao pia,
Budi kuuangalia.
761.
Idadi ikizidia,
Kazi tunaichafua,
Kiasi inatakiwa,
Kutosha ni maridhia.
762.
Kisha wanaozipewa,
Kazi zao wakajua,
Sio kutunukiwa,
Madudu yatatujaa.
763.
Wajuzi waliokuwa,
Kazi zao kuachiwa,
Siasa zikiingilia,
Taifa hukorofisha.
764
Ujira kuangalia,
Riziki ikatimia,
Kila inapopungua,
Uovu mpya huzua.
765.
Masoko yanatakiwa,
Kwa wakuu kuyajua,
Wasiishie tembea,
Pasina cha  kujiuzia.
766.
Balozi zingetakiwa,
Rasimu kuiandaa,
Kila nchi tukajua,
Nini cha kujiuzia.
767.
Nini cha kujiuzia,
Na rahisi kununua,
Wasiishi na kukaa,
kama vile matajiri.
768.
Hujisahau balozi,
Nchi wakawa hawawazi,
Wakaishia usingizi,
Na tija usiokuwa.
769.
Kufunzwa wanatakiwa,
Ujasiramali tabia,
Kazini kuutumia,
Wakistaafu pia.
770.
Bila hivyo hufulia,
Mengi yakawakimbia,
Na nchi kujikondea,
Minofu ikififia.
771.
Mawasiliano twajua,
Watu yanasaidia,
Na kilichobakia,
Unyonyaji kupungua.
772.
Hela zikichukuliwa,
Na wachache walokuwa,
kawaida inakuwa,
Ni vibaya kutumiwa.
773.
Vocha bei kupungua,
Na muda kuongezewa,
kiasi kitabakia,
Mengine kujifanyia.

774.
Dijito teknolojia,
Jinsi ninavyoelewa,
Urahisi yatakiwa,
Maisha kutufanyia.
775.
Ujanja ukipungua,
Gharama haitakuwa,
Mbadala kujaliwa,
Kawaida kurejea.
776.
Ila tukiwaachia,
Wajanja waliokuwa,
Pasina kuwa sheria,
Hili kuliangalia.
777.
Kwa miaka kama mia,
Mlaji kumrarua,
Hii ndiyo dunia,
Mabepari twawajua.
778.
Kompyuta Tanzania,
Budi kujitengezea,
Zetu zilizokuwa,
Kiswahili zatumia.
779.
Ni lugha iliyokuwa,
Kila mtu atumia,
Mwanzo wameanzia,
Wenye simu twasifia.
780.
Sasa ni kufatia,
Kompyuta kutumia,
Na mtandao ukawa,
Kiswahili kidedea!
781.
Vizuri tukijitoa,
Vyuo tutavifungua,
Kwa tovuti kutumia,
Afrika kuenea.
782.
Na ajira zikajaa,
Afika kufunzia,
Kiswahili kikakua,
Na uchumi kuinua.
783.
Nacho tusichojaliwa,
Viongozi wakujua,
Njia wanaotambua,
Wapi pa kuelekea.
784.
Vijiji kubwa hazina,
Kuvitunza vikafana,
Tena pasina hiyana,
Kwani tumevionea.
785.
Huduma nyingi zavia,
Kila mtu anajua,
Muongo unatakiwa,
Haya tuawapatia.
786.
Maji kutiririka,
Vijijini tunataka,
Waache kuhangaika,
Kinamama kuadhirika.
787.
Umeme kutochelewa,
Nyuma ukayafatia,
Gizani hatukuumbiwa,
Ni nani asiyejua.
788.
Nyumba nimeongelea,
Zastahili familia,
Kwa mbinu kujengewa,
Na ajira zikatoa.

790.
Hayo yakishakuwa,
Ndege yetu itapaa,
Mengine kuangalia,
Hali bora kufikia.
791.
Takwimu za Tanzania,
Watu shaka watilia,
Katiba ingetwakiwa,
Na hili kuliondoa.
792.
Ninachofikiria,
Mamlaka kuundiwa,
Na mtu isoingiliwa,
Kazi ikajifanzia.
793.
Kwa hivyo kuaminiwa,
Uhuru ikishajaliwa,
Jukumu ikalipewa,
Ukweli kupigania.
794.
Uongo kukaataa,
Na waongo kuumbua,
Mkuu hadhi akawa,
Katiba kumwangalia.
795.
Ya vyama yasiyofaa,
Hayo tutayaambaa,
Na ikulu ya kuzua,
Ukweli tukaujua.

796.
Ya tume yenye hadaa,
Yote tukayafichua,
Sensa bora kujaliwa,
Muongo kat ukiwa.
797.
Dawa tungejitambua,
Mbali tungeishakua,
Uizi uliingia,
Hakuna wa kuaminiwa.
798.
Katiba inatakiwa,
Wa jadi kuangalia,
Na msaada kupewa,
Vyao wakajiundia.
799.
Za asili tungetoa,
Na za kisasa kuzua,
Kama Wachina tukawa,
Uchumi tukajaliwa.

No comments:

Post a Comment