941.
Uungu wanaotaka,
Riziki kutugawia,
Au wanapoamua,
Riziki wakatunyima.
942.
Ila ni wewe hakika,
Lako linalofanyika,
Hawa wanhamanika,
Kuwa kile wasokuwa.
943.
Firauni ni amiri,
Yeye hakuihiari,
Kajitia ujibari
Baharini kuishia.
944.
Dharau waliojaa,
Na kiburi kujitia,
Yao yapate sinyaa,
Na ukomo kuingia.
945.
Heri kutoifungua,
Na shari kuwagawia,
Wenye njaa Tanznia,
Viongozi walokuwa.
946.
Ni maradhi waugua,
Ya uroho na tamaa,
Wanaolikimbilia,
Walijua hawawezi!
947.
Utajiri waabuduo,
Tuwaachie ya kwao,
Mitaji tutafutayo,
Mashaka sije kutiwa,
948.
Uhai nao tukiwa,
Hata nasi tajichumia,
Kukuza wasiojua,
Hawafai Tanzania.
949.
Ubadhirifu wajaa,
Uchungu hawajatiwa,
Vya kwetu wavitumia,
Na akiba waing'oa.
950.
Kukopa wamezoea,
Deni watuongezea,
Tunadhulumu jamaa,
Vitukuu kuachia.
951.
Si haki inavyokuwa,
Wengine twawaonea,
Kodi wanaojilia,
Mifupa ikabakia.
952.
Kwachana nao yafaa,
Haki tukajitendea,
Mwamala haitakuwa,
Vingine tukiamua.
953.
Jinsi tunavyosaidiwa,
Inashangaa dunia,
Kwanini tunafulia,
Hatuwezi endelea?
954.
Zowezi linatakiwa,
Pembeni kuwafagia,
Wasojali tasnia,
Wababaishaji wakawa.
955.
Michezo twaichezea,
Badala kwetu kufaa,
Ukubwa wanaolilia,
Kuongoza wafulia.
956.
Wanaokwaza afya,
Hali watu waugua,
Na wengine kujifiq,
Sio wa kuvumiliwa.
957.
Watatiza tasnia,
Ukubwa kung'ang'ania,
Pasi kupiga hatua,
Na ujira wajilia.
958.
Chajaa chao kibaba,
Kwetu wengine ni haba,
Vipi tuwe nayo mahaba,
Nchi kuisaidia?
959.
Keki wakiipakua,
kubwa wanajigawia,
Sababu wakizitoa,
Ni ngumu kutukatia.
960.
Uongozi kujifaa,
Wala sio kutufaa!
Masikini waumia,
Hali kwao sasa mbaya,
961.
Mikakati watumia,
Wenye nacho kuwafaa,
Fakiri aliyekuwa,
Azidi kupotezewa.
962.
Wanakula ya fakiri,
Pasina yao hiari,
Mnyonge kweli kafiri,
Nani kumsaidia?
963.
Dhiki huzivumilia,
Wakadhani aridhia,
Ila wakati hutua,
Vumbi akalitibua.
964.
Imani ilowakaa,
Laiki ni kutulia,
Hawapendi ya kuzua,
Wote yanayochafua.
965.
Mapagani wanakuwa,
Wale waliolaaniwa,
Shetani huwachagua,
Kuishi mwao kichwani.
966.
Na wao wakaamini,
Wadhani wana amani,
Iliyokuwa yakini,
Kiumbe hawajamjua!
967.
Maumivu twayakuza,
Na nchi twailemaza,
Kitu gani tutaweza,
Labda iwe miujiza.
968.
Kupewa twajivunia,
Hali twazidi lemaa,
Utumwani kurejea,
Hadi tunachekelea!
969.
Tunataka kusifiwa,
kwa misaada kupewa,
Nashindwa waelewa,
wanaolilalamikia!
970.
Vya wazazi watumia,
Watamba wajichumia,
Siku wakijiondoa,
Ukweli tutaujua!
971.
Daktari wamwonea,
Wao bora wajitia,
Akilini kuingia,
Gumu ninajionea!
972.
Haujengi ufahari,
Kaziye kuzua shari,
Na asiyetahayari,
Dunia hajaijua!
973.
Huo wa bure wadhifa,
kila pembe una nyufa,
Na kukosa maarifa,
Yakawa yetu maafa.
974.
Watakao abudiwa,
Shiriki wanaizua,
Nawe dawa waijua,
Dozi ungewapatia.
975.
Ndiwe mwenye kuamua,
Tuepushie Tanzania,
Amani tukaeilea,
Wasia nawapatia.
976.
Mkoa huru kuamua,
Kupu'za au kusikia,
Mola namshuhudia,
Mmoja aliyekuwa.
977.
Kazi si kung'ang'ania,
Ila mamlaka kugawa,
Watu kujiamlia,
Kesha wakaiangalia.
978.
Na katiba yatakiwa,
Msingi kushindilia,
Haya kuyafafanua,
Pasiwe nayo mashaka.
979.
Watawala watakiwa,
Kwanza nao wakajua,
Juu wanapokuwa,
Hilo wamekasimiwa.
980.
Wa chini wakatambua,
Matajiri watakuwa,
Na ajira waitoa,
Kwa wanaochaguliwa.
981.
Uchama rahisi njia,
Shughuli kuangalia,
Kitaifa na kimkoa,
Watu wakaendelea.
982.
Ni haramu kuchangia,
Watu kutoendelea,
Kwa vituko na hadaa,
Na ukubwa kupigania.
983.
Katiba inayotakiwa,
Yapo mengi kuamua,
Na moja la kulijua,
Watu ndio walo juu.
984.
Wapewao madaraka,
Sheria kuziandika,
Wasije katiba baka,
Juu wao kudhania.
985.
Angalizo nalitoa,
Hilo ndilo linazua,
Udiktata mbaya,
Afrika tukazua.
986.
Magharibi yatuvaa,
Na upofu kututia,
Mchina wamhofia,
Nasi atatuchukua.
987.
Akili wangelikuwa,
Haki wangeliitumia,
Vyetu walivyotwibia,
Fidia wakaitoa.
988
Mola kawageukia,
Njaa kwao yaingia,
Na ajira zapotea,
Kwa Afrika kuonea!
989.
Ni imani kutangulia,
Wenye heri kuamua,
Imani kuichangia,
Wala si kuitumia.
990.
mwenyewe kujifagilia,
Na kisha uakdhania,
salama utabakia,
Uranium wachezeao,
991.
mabahau kutufanza,
Ili wachume wao,
mbali wanaojitunza,
Hakika kina mfamao,
992.
hawafai maliwaza,
Sensa wanaochezea,
na takwimu kuzipika,
Hila wanayoitia,
993.
Zinachafua hadaa,
Na uongo kuzagaa,
Vitisho ikavitia,
Shetani aone haya!
994.
Dua nnajisomea,
Hitima kumalizia,
Mwenyezi kutujalia,
Salama kumalizia.
995.
Katiba inatakiwa,
Kufaa miaka mia,
Ikiweza kuzidia,
Siye tutafurahia.
996.
Kazi tunayoifanya,
Isije kuwa na mwanya,
Wajanja wakijikusanya,
Uzaini wakatia.
997.
Mabepari kuwafaa,
Pia nao wajamaa,
Wote tukachangia,
Taifa letu kukua.
998.
Tajiri kufurahia,
Na masikini nao pia,
Yao kwa kuangaliwa,
Pasina ya kuonewa.
999.
Wazee kushabikia,
Na vijana kuridhia,
Katikati itakuwa,
Pande kutoegemea.
1000.
Rushwa ni jambo baya,
Kwan chi kuvumilia,
Hukua na kuenea,
Hadi nchi ikaoza.
1001.
Katiba natarajia,
Muongozo itatoa,
Vita kuitangazia,
Rushwa hapa Tanzania.
1002.
Ya chama kwa kuanzia,
Kama chama kinatoa,
Au ikaipokea,
Kufutwa ingelikuwa.
1003.
Visafi vikabakia,
Na uoza kuondoa,
Nchi ikaheshimiwa,
Na muumba kuijalia.
1004.
Ya mmoja kuzuia,
Kwa k uitunga sheria,
Rushwa atayepokea,
Jela kwenda kuingia.
1005.
Gerezani akatiwa,
Kazi ngumu kuzilea,
Mazao kutupatia,
Nchi ikaendelea.
1006.
Rushwa anayepokea,
Korokoroni kukaa,
Funzo akaandaliwa,
Ubaya wake kujua.
1006.
Elimu ataipewa,
Mitano ‘kitumikia,
1,007.
Waovu kuichukia,
Na wema kushangiia,
Kwa haki kutangulia,
Kila itachoamua.
1,008.
Uongo ikatambua,
Huwaumiza raia,
Daima kweli ikawa,
Nchini yashuhudiwa.
1,002.
Maadili kuwaniwa,
Utumishi bora kuwa,
Wana wkajitolea,
Nchi yao kutetea.
1,009.
Tuijenga Tanzania,
Kesho tukajivunia,
Wana wakatusifia,
Chema kwa kuwaachia.
1,004.
Taifa hili kung'aa,
Hata nje kusifiwa,
Mfano wakautoa,
Iwe kama Tanzania.
1,010
Namshukuru Alaa,
Watu mwenye kunyanyua,
Na kuondoa udhia,
Taifa bora likawa.
1,011.
Kwa nafasi kunachia,
Na mimi nikachangia,
Moyoni yaliyokuwa,
Kama yatakubaliwa!
No comments:
Post a Comment