Thursday, November 17, 2011

Muswada wa katiba ni waCCM na serikali yake na hauna nia njema na Watanzania wa sasa na wajao......

Kwanini tunasema katiba ni mali ya wananchi ?

HUFIKA wakati katika historia ya nchi ikawalazimu viongozi waliopo kukaa pembeni na kuwaachia wananchi madaraka au mamlaka ya kufanya maamuzi muhimu ya kitaifa. Mojawapo ya wakati kama huo ni pale nchi inapotka kuwa na katiba mpya. Kwa kuwa wananchi ndio wenye sauti ya mwisho na maamuzi makuu katika suala hili ni uungwana, haki na kuona mbali na mbele kwa viongozi waliokuwepo kusalimu amri kwa wananchi na kuwakabidhi kupitia watu ambao wananchi wenyewe watakaowachagua kuwawakilisha katika kuandaa utaratibu mzima toka kuanza hadi kumaliza kazi ya kupata mchakato wa njia na namna za kuipata katiba na vilevile upatikanaji wa toleo la mwisho la katiba mpya litakalopigiwa kura na wananchi.

Hii ni hatua inayohitaji viongozi wanaojiweka zaidi kama viongozi wa kitaifa na wafanya maamuzi makuu yatakayoathiri maisha ya kizazi hiki na vizazi vijavyo kwa wema au ubaya. Wanaoshindwa kufanya hili hawatendei haki wajibu na majukumu wanayostahili kuyabeba kama viongozi wa watu na nchi yao.

Uongozi unaoshindwa kutambua kwamba muda wa KUSALIMU AMRI KWA WANANCHI WAKE umefika ni uongozi wenye hatari ya kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ni uongozi usiotakia kheri kizazi kilichopo na vizazi vijavyo katika nchi husika.


Ukubwa mlionao

Ukubwa mlionao, mmepewa na wananchi,
Hawa ndio waamuao, hatima yenu na nchi,
Na muda wautakao, huwapeleka benchi,
Wafanye maazimio, kula mbivu au mbichi,
Ukubwa muutakao,kwa nachi na upanchi,
Hamjui mfanyayo,si wananchi ni wenyenchi,
Ni hasama mleltao,wana waje enda uchi,
Hayo kama matamanio,iwe kucha haukuchi,
Fanyeni wayatakayo,Tanzania wananchi,
Na siyo muyatakayo,mlio kwenye makochi,
Taabu si mjuao,wala hamli vibichi,
Sio muhangaikao,ni rahisi zenu mechi,
Na sio muelewao,nini hatima ya nchi!


Akizungumzia uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.

Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.

Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.

Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.

Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.

Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.

Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.


UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.

Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.

Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.

Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.


CCM na wakewenza Unguja

Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.

Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.

Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.

Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.

Viongozi wa dini

Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.

Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.

Makampuni na taasisi na katiba

Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.

Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.

Sunday, November 13, 2011

Viongozi, serikali Tanzania vyadhamiria Mapinduzi ya Kikatiba

WAKATI tayari wabunge wanashinikizwa kuusoma mswaada wa katiba mpya kwa mara ya pili badala ya kusomwa mara ya kwanza, ninachukua fursa hii kuwaasa viongozi na wabunge wetu kwamba kitendo cha kuusoma mswaada huu kama unaosomwa mara ya pili haitakuwa tofauti na wao kuipindua katiba ya nchi na kosa hilo ni sawa sawa na mapinduzi ya kijeshi, tofauti ikiwa yale ya kijeshi watu wengi watakufa siku hiyo hiyo, wakati haya ya kikatiba Watanzania wote watakuwa wanauawa taratibu na kimya kimya.

Watanzania wana haki kwa kutumia wawakilishi wao wa kweli na halali kuhusiana na suala la katiba na sio wanafiki na vibarakala wa wale walioko madarakani, kuchukua hatua zote za kisheria ni kiharakati ili 'wanaoazimia kuipindua' katiba kinyume cha sheria wanachukuliwa hatua zinazostahili. Na sio tu serikali imeamua kuipindua katiba, bali inawaziba mdomo na masikio wananchi ili wasijue kinachofanyika kwa kuwatumia wale waliochaguliwa kulinda haki na maslahi ya watawala na sio ya watawaliwa!

Aidha, damu, dhiki na machungu yoyote yatakayosababishwa na kuusoma na kuupitisha mswadaa huu, laana yake iwaangukie viongozi wa Tanzania wa zamani na wa sasa.

Tunajua ugumu wa viongozi wa Afrika na hasa hawa wetu wa Tanzania kusalimu amri. Inatisha pale viongozi hao tena wanaposemekana ni wale wanaosalmi amri kwa Mwenyezi Mungu, lakini labda si hawa wa sasa...na kama wanalaghaiwa na wale wanaowashauri kwa sababu binafsi za washauri hao, basi huu ni wakati muafaka wa hususan rais, kusalimu amri na kuwarudishia Watanzania haki yao ya kikatiba ya kuwa ndio wenye mamlaka na madaraka ya juu kabisa kwenye suala kama hili na sio yeye rais. Anachoshauriwa kukifanya rais kwa hivi sasa ni sawa na 'kuwapindua Watanzania' kwa kuipindua katiba yao iliyopo hivi sasa ambayo ndiyo inayosema wao ndio wenye sauti ya mwisho juu ya katiba na sio rais.


Kwa kuzingatia hayo hapo juu, ni muhimu awali ya yote kuweka jambo moja muhimu kuliko yote sawa hapa. Je, ni rais au ni wananchi wenye haki ya kusimamia mchakato wa katiba mpya ? Je, rais si kiongozi wa seriikali taasisi ambayo ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Na rais huyo huyo sio mwenyekiti wa chama tawala ambacho ni mmoja wa wadau katika suala hili la katiba? Katika hali kama hii haki na uadilifu uko wapi? Ni katiba gani inayomruhusu rais kuwapora wananchi haki yao ya kuwa ndio walio na mamlaka na madaraka ya juu na ya mwisho kwenye masuala kama haya?


Kuna mambo kadhaa ambayo ninafikiri ni muhimu
kuwekwa wazi na ikiwezekana kutekelezwa hata kabla ya Tanzania kuwa na katiba mpya.

1. Mosi ni ufafanuzi wa nani ndiye mwenye sauti na maamuzi kuhusu mchakato wa katiba mpya kwa mujibu wa katiba tuliyonayo, yaani, ni nani kati ya wananchi kupitia chombo au vyombo vyao halali vya uwakilishi vilivyopo au kitakachoundwa au ni serikali na kiongozi wake. Utata unakuja pale tunapobaini kwamba serikali nayo pia ni mdau katika mchakato huu. Na kwamba si haki kwa chama au serikali kujipa mamlaka au madaraka ambayo hawastahili kuwa nayo, kwani huko ni sawa na kupora mamlaka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kutumia silaha.

2. Haki ya Kuandamana na Maandamano. Tofauti na katiba ya sasa inavyoruhusu, utawala wa sasa, unadai kwamba watu hawana uhuru wa kuandamana na kufanya maandamano. Pamoja na kuwatia ulemavu wa maisha baadhi ya Watanzania wasio na kosa, usalama wa taifa na vyombo vya dola hususan FFU, vinatumika kuvuruga amani na kuharibu mali za Watanznia. Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.

3. Haki ya kukutana na kufanya mikutano. Ilivyo hivi sasa kama hapo juu inaonekana Watanzania hawana haki ya kukutana na kufanya mikutano inayohusu maisha na maendeleo yao na mitaa na vijiji vyao ila pale wanaporuhusiwa na chama tawala kupitia serikali yake iliyoko madarakani.Kazi ya usalama wa taifa na vyombo vya dola si kuzuia maandamano na mikutano bali kuweka taratibu za kuhakikisha wanaofanya mikutano na maandamano hayo wana ulinzi na usalama wa kutosha.

4. Mikoa na haki za wakazi wa mkoa. Hali ilivyo sasa chama tawala na wale wanaoteuliwa kuwa viongozi wa mikoa wanachaguliwa sio kwa uwezo wao wa kimenejimneti na kuchangia maendeleo ya wakazi wa mkoa husika bali kwa sababu za kisiasa. Ni mfumo wa kikoloni ambao mkoloni mkuu anachagua wakoloni wa kumasaidia kuidhulumu na kuinyonya mkoa husika. Tz. kwa mfano mikoa ya Mwanza na Arusha hivi leo. Mikoa inastahili kutawaliwa na chama ambacho kina wabunge na madiwani wengi katika mkoa husika na sio vinginevyo. Aidha, kukidhi changamoto za kimaendeleo zilizopo wakati umefika kwa mkoa kuwa na Waziri wake mkuu na baraza lake la mawaziri wa mkoa husika ili kuimarisha uhuru, umoja, haki na kuharakisha maendeleo ya mkoa husika.

5. Endapo kiongozi anatoa AHADI na anashindwa kuzitekeleza nini kifanyike dhidi yake na wanaohusika kwa ujumla?

6. Nini liwe jukumu la serikali na wanasiasa kuhusu mustakabali wa vijana wasio na ajira, wamachinga na waendesha biashara ndogondogo.

7. Haki ya vyama kuungana. Mpaka sasa haieleweki kwanini kuna ugumu kwa vyama vya kisiasa kuungana ili kupunguza utitiri wa vyama nchini ambao hausaidii kuimarisha mfumo wa vyama vingi nchini bali kuudhoofisha zaidi na zaidi.

8. Haki ya Mgombea huru nchini. Mpaka sasa sheria imepindwa na katiba imepinduliwa kinyemela kwa kumnyima haki Mtanzania anayetaka kugombea uchaguzi bila kufungamana na chama chochote cha kisiasa.

9. Apartheid ya viongozi kutibiwa nchi za nje wakati walalahoi wanakufa kwa kukosa fedha za kuchangia katika zahanati na mahospitali sehemu mbalimbali nchini iendelee au ife kwa kuwa na hospitali bora zaidi nchini na madakta wasio na kazi kwenye nchi zenye matatizo ya kiuchumi hivi leo duniani.

10. Nini iwe nafasi ya upinzani katika uongozi wa nchi, mikoa, wilaya na majimbo? Na je tutarahisishaje vyama mbadala kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika sehemu mbalimbali nchini.

11. Vyama viendeshwe vipi ili vipate mapato halali na sio kutegemea hazina ya serikali au kupata fedha kupitia njia ambazo zitahatarisha uhuru na utu wetu.

12. Vipi vinastahili kuwa vyombo vya habari vya wananchi na vipi vya serikali na chama tawala. Mkurugenzi achaguliwe vipi na nani? Uhuru wa vyombo hivyo utahakikishwaje?

13. Nini iwe kazi za majeshi yetu wakati wa amani? Yatashirikishwaje katika uzalishaji mali, huduma za jamii, biashara, uchimbaji madini ili kuhakikisha rasilimali za Watanzania hazipewi sawa na bure kwa wageni eti tu kwa sababu hatuna utaalamu na mitambo ya kufanya shughuli fulani?

14. Nini yawe majukumu ya usalama wa taifa ili uwe na tija zaidi katika maendeleo ya kiuchumi na kiteknolojia ya Watanzania kuliko ilivyo sasa. Na je ni sahihi usalama wa taifa kuchunguza viongozi wa zamani au wa upinzani kikatiba na kisheria?

15. Je, mamlaka ya Rais kuteua watu kama wakuu wa polisi, wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya, majaji, mahakimu, wabunge wasiochaguliwa ni jambo zuri na linaloimarisha demokrasia au ni baya na linalodhoofisha uhuru, haki za binaadamu na demokrasia. Nini kifanyike kumaliza utata huu?

16. Je, Soko huru linastahili kuingiliwa na viongozi wa serikali ili kutafuta umaarufu wa bei rahisi? Nini kifanyike kama tumeshakubali kuwa nchi ya kibepari na soko huru. Nchi ifuate mfumo gani wa kisiasa bora kuliko ubepari na ukomunisti kesho na keshokutwa? Nini kimilikiwe na wageni na watu binafsi au wanajamii husika au serikali au ubia wa aina hii au ule?

17. Je, tunahitaji kikomo cha safari za nje ambazo kiongozi aliyeko madarakani anaweza kuzifanya katika kipindi chake cha miaka 5?

18. Je, ni magari ya aina gani na gharama gani wanastahili kuwa nayo viongozi wa serikali na wabunge na watumishi wa umma?

19. Ni vipi maji ya mito, maziwa, bahari, ardhini na mvua yanaweza kupatikana na kuhakikisha upatikanji wa maji safi kwa Watanzania sehemu zote za nchi na wakati wote?

20. Je, ni wanasiasa au watu wenye utaalamu fulani, k.m. walimu, wahadhiri na madaktari ndio wanaostahili kulipwa vizuri zaidi? Na kwanini mwanasiasa asilipwe kutokana na tarafu au kazi aliyoisomea na cheo anachostahili kuwa nacho wakati huu?

KIMSINGI, hayo hapo juu ni machache tu katika kero, vilio, matamanio, ndoto na matarajio ya Watanzania na hususan vijana ambao ndio wazazi na wenye nchi wa kesho kuhusu jinsi ambavyo wangelipenga kuona suala hili la katiba likishughulikiwa kama inavyostahili na sio kwa kutumia ujanja, maguvu, mabavu, uzaini, uzandiki, ubabe na uhuni huku wanaofanya hivi wakijua fika kwamba njia wanayotupeleka ni ya shari na siyo ya kheri!!!

Kama Rais, waziri mkuu, mawaziri, wabunge, jaji mkuu, mwanasheria mkuu na washauri wengine wa waheshimiwa wana nafasi ya kuonesha hekima na busara basi ni leo Jumatatu, tarehe 14, Novemba 2011 ni KUSALIMU AMRI NA KURUHUSU MSWAADA HUU USOMWE MARA YA KWANZA NA SIYO YA PILI!!!

Saturday, May 28, 2011

+1,2,3,4,5,6,7,8,9,10+++

Meta Meta Online.

4 = Baraza + Katiba mpya +

Taifa +mchakato + mkutano +

mwananchi + raia+ Haki +

Mmiliki + Tajiri + Mwajiri

+26,27,28,29,30,31,32,33,34,3

5,36,37,38,39,40,41,42,43,44,

45,46,47,48,49,50. + Tanzania

+Watanzania + raia +mzawa +

Uingereza + Marekani +Rais +

Mawaziri + Mkoa + Wabunge +

Rasilimali + mali asili + Mkoloni

+Wawakilishi + Mkulima

+Mfanyakazi +Daktari

+Umaskini, Ujinga na Maradhi

+Nesi+ HakiKatiba

+1,2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,

14,15,16,17,16,19,20,21,22,23

,24,25.

[1],2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,

14,15,16,17,16,19,20,21,22,23

,24,25,26,27,28,29,30,31,32,3

3,34,35,36,37,38,39,40,41,42,

43,44,45,46,47,48,49,50.


Enable transliteration?

Friday, May 27, 2011

1. MKULIMA.

TULIPOPATA uhuru ilisemekana eti Uti wa mgongo wa taifa letu ni kilimo. Mkulima

na vijiji vimebadilika kidogo sana toka tupate uhuru. Ingawa tumejenga kiasi mijini lakini vijiji vimesahaulika.

Serikali na chama tawala vilipoua ushirika halisi na kuleta ushirika wa kisiasa

mkulima aliathirika vibaya sana.




Vijiji vya Ujamaa lilikuwa ni wazo zuri lakini watendaji wa serikali wakatumia fursa

hiyo kuchukua ardhi nzuri ya vijiji na kuwahamisha wakulima karibu na barabara

au kwenye maeneo yasikokuwa na rutuba hata kidogo.


Mamlaka nyingi z amazao zilizoanzishwa zilimnyonya na kumuibia zaidi mkulima

kuliko kumsaidia na wanasiasa taratibu wakavila na kuviua vyama vya ushirika.

Soko huria na siasa za kiliberali zilipoingia mkulima tu ndiye ambaye hakuruhusiwa

kuuza mazao au bidhaa alizozalisha nchi za nje. Na hadi wa leo soko la mkulima

limekuwa likivurugwa na serikali na wanasiasa. Tujiulize:


i. Kama tumekubali soko huru jambo hilo halimhusu pia mkulima;
ii. Kwanini tusimruhusu moja kwa moja mkulima kuuza mazao yake nchi

za nje kwa taratibu atakazopanga yeye na wenzake;
iii. Je, tukimhakikishia mkulima soko linalomlipa bei za kishindani kilimo

hakitafanikiwa;


iv. Je, VICOBA vya kilimo haviwezi kuendeshwa kwa namna ambayo sio

tu ni benki za kijamii, bali pia ni chombo cha bima na hifadhi ya mkulima (Social

security fund);
v. VICOBA vya wakulima vikishirikiana na benki za maendeleo ikiwemo

hiyo ya kilimo haziwezi kujipanga ili kuhakikisha wakulima wengi iwezekanavyo:
-wanakopeshwa matrekta;
-wanapata mbegu, mbolea na mahitaji yao mengine kirahisi na kwa namna

isiyowagharimu fedha yote kwa wakati mmoja;
-wanasaidiwa kutafuta masoko kabla ndani na nje ya nchi;
-wanafikishiwa hutuma muhimu vijijini kama vile maji, umeme na miundombinu

kwa kutumia pia idara ya VICOBA itakayopewa jukumu la utoaji huduma muhimu

kijamii na kibiashara;
-Je, VICOBA, Benki ya Kilimo, wafadhili na serikali itawasaidiaje wakulima kuwa

na nyumba bora na huduma zote muhimu ili pamoja na kilimo vijiji viweze

kuendesha pia biashara ya utalii wa vijijini na kilimo;
-Kila inapowezekana VICOBA na BENKI ya Kilimo visaidiwe uanzishwaji wa

viwanda vidgo vitakavyowasaidia wakulima kuuza unga sembe badala ya kuuza

mahindi; kuuza ngano iliyosagwa badala ya mali ghafi ya ngano; kuuza mchele

badala ya kuuza mpunga na kuuza mafuta ya kupikia badala ya kuuza alizeti na

nyonyo;
-Je, hivi wizara ya Kilimo na chakula inatakiwa iwe na wafanyakazi wanaoishi na

kuonesha mifano vijijini au wapunge upepo wa bahari kama sio wa bonde la

TAZARA?

-Na yote haya yatazungumzwa na nani kama sio mwakilishi halali na

anayetegemewa kuzungumza kinachotakikana kama sio mwakilishi wa

wakulima/wanavijiji;

Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie

kwake au sio?


[1],2,3,4,5,6,7,8,9,10,11,12,13,

14,15,16,17,16,19,20,21,22,23

,24,25,26,27,28,29,30,31,32,3

3,34,35,36,37,38,39,40,41,42,

43,44,45,46,47,48,49,50.





HakiKatiba 2011:

WAKULIMA wetu sio wajinga. Wanasiasa waliotaka kuwageuza wakulima kuwa punda wao na kuchuma kupitia migongo yao badala ya wao kuwa uti wa mgongo wa taifa ndiyo zilizotufikisha hapa tulipo leo!

2. MFANYAKAZI SEKTA BINAFSI.

MFANYAKAZI wa sekta bnafsi sekta inayochukua nafasi ya ile ya umma anahitaji

pia kuwezeshwa ili isionekane kwamba sikuzote Mtanzania ni mtu wa kunyonywa,

kunyanyaswa na kudharauliwa tu.



Mfanyakazi huyu ni lazima alipwe mshahara unaoweza kukimu mahitaji yake yote

ya msingi na kudunduliza akiba kwa ajili ya dharura na mahitaji yanayokuwa

kutokana na kukua kwa familiaa.



Hali ilivyo sasa ni kuwa hata wale wafanyakazi wa tabaka la pili ambao juzi na jana

walikuwa na uwezo wa kubeba gharama za utunzaji na uendeshaji chombo cha

usafiri hivi leo wana tishio la kushindwa kumudu kutunza magari yao.

Ukija hilo daraja la chini hali ndio mbaya kabisa na katika nyumba nyingi lishe ni

duni, fedha sikuzote hamna na mahitaji mengi ya msingi ni vita kuyamudu.



Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie

kwake au sio?



HakiKatiba 2011: Mfanyakazi kamili ni yule ambaye anatimiziwa mahitaji yake yote ya msingi. Na mwajiri adilifu ni yule anayejua kuwashibisha kwanza wafanyakazi wake kabla yeye mwenyewe hajala.

3. DAKTARI.

NCHI nyingi za Kiafrika zina kichekesho kimoja kikubwa. Kichekesho hicho sio

kingine ila ni kile cha wanasiasa (wengi wakiwa hawana hata nusu ya kisomo cha

madaktari) kulipwa mishahara mikubwa kuliko jeshi hili muhimu la kuokoa maisha

ya raia wetu.

Ndiyo maanake hata madaktari nao wanataka kuingia kwenye siasa ili

waondokane na mishahara njaa. Je, hivi kwa akili na upeo wetu daktari anastahili

kulipwa mshahara mdogo kuliko diwani,mbunge, waziri au hata dereva au

mtumishi wa ndani wa waziri kweli ? Na jamaa hawa wakitimkia nje hivi kweli kilio

chetu cha uzalendo kitasaidia kitu? Sio kwamba wakati umefika wa wabunge,

mawaziri kulipwa mshahara unaolingana na elimu, ujuzi na vyeti vyao? Badala ya

nafasi hizo kuwa za kwenda kujilimbikizia utajiri ziwe ni changamoto kwa wale

wanaotaka kuacha kazi zao au biashara zao kuingia kwenye siasa ? Na kwamba

hadi wa leo hatujapindua kichwa -chini na miguu-juu ssuala hili la mishahara. Kwa

maana ya kuwa sio wanasiasa waliostahili kulipwa mishahara mikubwa bali

washiriki moja kwa moja kwa vitendo kwenye sulubu na maumivu ya kuwajenga

Watanzania kiafya, kiakili na kimwili ili wachangie si haba pato la taifa na

maendeleo ya jamii zao na nchi yao?

Tanzania laiti ingelikuwa na mikoa huru kiuchumi na kijamii serikali za mikoa na

wakazi wa mikoa husika wana uwezo wa kuzifanya hospitali zetu kuwa bora kiasi

ambacho wagonjwa wengi katika nchi mbalimbali za Kiafrika wakaja hapa kutibiwa

na kuuguzwa badala ya kupelekwa nchi za nje ? Na hili likifanyika ni kwamba

mishahara, marupurupu yenu na kipato chenu kwa ujumla kitaongezeka na

hamtakuwa na sababu ya kukimbilia nchi za nje !

Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima


avutie kwake au sio?




NCHI inayowaheshimu madaktari na manesi wake na kuwa na vifaa vya kisasa vya tiba, wafanyakazi wachapakazi, mazingira mazuri kwa wafanyakazi na wagonjwa mahospitalini inaweza kupata fedha za kigeni kutokana na kuja kwa wagonjwa wengi kutoka nchi jirani na za mbali kutibiwa hapa kwetu.

4. NESI.

MANESI wetu wanalaumiwa hivi leo kwa kila jambo lakini ukangalia kwa undani ni

suala la mishahara tu na maslahi.



Kwa mtu anayefanya kazi wakati mwingine masaa 10 au zaidi kwa siku,

anayekosa usingizi mara kwa mara na anayetakiwa kutoa huduma ambazo wengi

wetu tutafikiri mara mbili kukubali kuzifanya wakati umefika kwa kweli kuangalia

uwezekano wa kuwa na kima cha chini cha mshahara ambacho kitawavutia

wanawake na wanaume wenye wito kufanya kazi hii ya unesi kwa huruma,

mapenzi na uvumilivu.


Je, wewe nesi unadhani kuna mtu anaweza kuwakilisha kilio, mahitaji, matakwa na

matarajioa yako ila nesi mwenzako uliyemchagua kwenda kusema unachokittaka

kiwekwe hadharani?


Zingatia kuwa serikali na wananchi wa Tanzania wana uwezo wa kuzifanya

hospitali zetu kuwa bora kiasi ambacho wagonjwa wengi katika nchi mbalimbali za

Kiafrika wakaja hapa kutibiwa na kuuguzwa badala ya kupelekwa nchi za nje ? Na

hili likifanyika ni kwamba mishahara, marupurupu yenu na kipato chenu kwa

ujumla kitaongezeka na hamtakuwa na sababu ya kukimbilia nchi za nje !



Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie

kwake au sio?



NCHI inayowaheshimu madaktari na manesi wake na kuwa na mazingira mazuri kwa wafanyakazi na wagonjwa mahospitalini inaweza kupata fedha za kigeni kutokana na kuja kwa wagonjwa wengi kutoka nchi jirani na za mbali kutibiwa hapa kwetu.



HakiKatiba 2011:
Hospitali zetu zikiwa nzuri, daktari na manesi wetu wakaridhika tunaweza kupata mabilioni ya fedha za kigeni!

5. MWALIMU.


MWALIMU kwenye miaka ya 1960 mara tu baada ya mkoloni kuondoka

walipendwa, kuaminiwa na kuheshimika lakini sio leo.

Je, tuanwezaje kurudisha upendo, imani na heshima kwa walimu hapa Tanzania?

Kilichofanyika hadi kufikia hapa ni kwamba wanasiasa waliamini kwamba wao ndio

wanaostahili kulipwa mishahara mizuri kuliko walimu wetu. Na kwamba ualimu si

kazi ya maana, wanaotaka waingie na wasiotaka watoke kirahisirahisi tu.

Matokeo yake ndiyo hayo ya kuporoka kila siku viwango vya elimu iwe ni msingi,

sekondar au high school!




Usahihishaji mitihani ndao unakuwa wa kibabe, kinuni na unaochangia

wasahihishaji kuondoka na zigo la madhambi kwa sababu ya kukosa kutenda haki

kwa watahiniwa. Hivi leo anayetegemewa kufaulu anaweza akafeli na mtu wa

kufeli akafaulu eti kwa sababu za kiufundi au kiteknohama. Lakini ukweli ni kuwa

upo uwezekano mkubwa wa haki sasa kununuliwa na wengine kudhulumiwa.



Tatizo ni mfumo wa usahihishaji uliopo ambao hauna wakati mwingine 'local

external examiner' na 'external examiner' kutoka nchi za nje ili kukamata uhalifu

huu katika 'sampling' itakayofanyika kiufundi na kijanja.

Lakini pia malipo kwa wasahihishaji yanapokuwa kidogo au wanapokuwa

wanapunjwa na maofisa husika au wanapokosa hazi zao nyingine kama wasahihi

shaji hili ni jambo la kutegemewa.


Lakini kubwa zaidi ni lile la kutaka kuitawala nchi nzima kutoka Dar es salaam.

Ninaamini kwa wingi wa shule tulizonazo leo wakati umefika wa kuwa na Bodi za

Mitihani za Mikoa ambazo zingeliandana uzuri sana na lile wazo la kuwa na

serikali huru kiuchumi na kijamii za mkoa. Mitihani itakaposimamiwa katika ngazi

ya mkoa au kanda kwa kuanzia itarahisisha usahihishaji wake na matumizi ya

wasahihishaji/waangalia mitihani toka mikoa mingine na nchi za nje.

Lingine ni lile la kurudisha MItihani yetu yote katika nchi zetu za Afrika Mashariki

iwe chini ya Bodi moja ya Mitihani ya Afrika mashariki kama ilivyokuwa East

African Cambridge enzi hizo!


Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima av


utie kwake au sio?



HakiKatiba 2011 Nchi isyowathamini na kuwalipa mishahara mizuri maprofesa, wahadhiri na walimu wake na badala yake ikakufuru kuwalipa wabunge, wanasiasa na viongozi wa serikali vizuri kuliko kundi hili na mengine kama haya lisahau kabisa kuondokana na umaskini, ujinga, maradhi na kuwa nyuma kimaendeleo.

6. MHADHIRI, PROFESA.


UKIKUTANA na maprofesa wetu ambao walikuwa wakimuogopa Mungu na kuishi

kimaskini kwa tumaini kuwa mishahara na pensheni zao zingeliwasaidia uzeeni,

aghalabu utatamani kulia.



NI maprofesa na wahadhiri ambao walimwibia mwajiri wao muda au kutumia utafiti

au ushauri kujitajirisha wao binafsi ndio wenye maisha mazuri.

Ipo haja ya kuangalia upya mishahara ya maprofesa na wahadhiri wa vyuo vikuu ili

tupate kilicho bora kutoka kwa na wanafunzi wao. Hivi leo, kwa kiasi kikubwa ni

kwamba tunajidanganya kwamba tunawalipa na wao wanadanganya wanatimiza

wajibu wao.



Njia mojawapo ya kuongeza mishahara na marupurupu ya wasomi hawa ni

kuhakikisha vyuo vikuu vinakuwa na miradi mizuri na toshelevu na endelevu

itakayoingiza kipato cha ziada kitakachotumiwa kwa maslahi ya walimu na

wafanyakazi wengine wa vyuo vikuu, kwa mfano, katika masuala ya kodi za

nyumba, usafiri na manunuzi ya vitabu na visaidizi vingine vya elimu na kisomo.



Namna nyingine ya kuongeza kipato kwa wafanyakazi wa vyuo vikuu vyetu ni

kuvitengea bajeti tosha ya utafiti kazi ambayo itafanywa na wote, walimu kwa

wanafunzi na mwisho wa siku wote watanufaika na kupunguza sana kilio cha

kipato na maslahi. Hili lal utafiti linaendana na matumizi ya ushauri wa walimu na

maprofesa wa vyuo vikuu badala ya serikali zetu kushauriwa na watoto wa mjini au

watumishi wa umma wakiwemo makatibu wakuu na mawaziri wenyewe kufanya

mipango ya kuwa na washauri wa kupanga toka ndani na nje ya nchi.



Endapo kila Mkoa nchini utakuwa na Chuo Kikuu chake cha umma, mishahara na

maslahi ya maprofesa na wahadhiri yana uwezekano mkubwa zaidi wa kuwa bora

na ya kuridhisha zaidi kwa sababu kwanza watakuwa kwenye mikoa ambayo si

ghali kama Arusha, Mwanza, Dodoma na Dar es salaam.



Sio tu kipato na maslahi ya maprofesa na wahadhiri yataongezeka bali hata

maendeleo ya kielimu, kijamii, kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa na kiteknolojia ya

mikoa husika itakwenda kwa kasi zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.



Na hili linawezekana kwa kuwatumia maprofesa na walimu waliopo hivi sasa na

kugawanya vitivo au fani za masomo mbalimbali ili Chuo Kikuu kimoja kisiwe na

zaidi ya fani 2-3 tu!



Isitoshe kuna maprofesa na wahadhiri wengi tu wasio na kazi kwenye nchi za

Ulaya Mashariki, Urussi na jamaa zake, Ireland, Spain, Portugal na hata Marekani

kwenyewe.



Yote haya yanaweza tu kufanikiwa ikiwa ni wahadhiri na maprofesa wenyewe ndio

watakaokuwa wawakilishi katika Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya

2011.



HakiKatiba 2011 Nchi isyowathamini na kuwalipa mishahara mizuri maprofesa, wahadhiri na walimu wake na badala yake ikakufuru kuwalipa wabunge, wanasiasa na viongozi wa serikali vizuri kuliko kundi hili na mengine kama haya lisahau kabisa kuondokana na umaskini, ujinga, maradhi na kuwa nyuma kimaendeleo.

7. MHANDISI.

MIAKA kadhaa Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa Afrika

kuwa na Kitivo cha Uhandisi kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Vyuo kadhaa vya ufundi ukiachilia mbali vile vya VETA vilivyokuja baadaye pia

vilianzishwa kwa madhumuni kama hayo.

Katikati hapa sera na mwelekeo wa kisiasa umeua au kulemaza sana taasisi zote

ikiwmo viwanda, maabara, vyombo vya usafirishaji na uchukuzi kiasi ambacho

mustakabali wa wahandisi na mafundi wengine uko mashakani.

La kusikitisha ni kuwa Mhandisi wa Kitanzania hadi wa leo hajaweza kutengeneza

hata sindano achilia mbali pasi, balbu, pampu ya maji, baiskeli, redio, televisheni

achilia mbali mashine na mitambo inayotakikana kwa uzalishaji hili au lile.

Serikali hii imebweteka mno kuhusu suala la uhandisi na nafas yake katika kutumia

kwa vitendo sayansi, teknolojia na teknohama katika miaka hii ambayo kuna

wahandisi tele na maprofesa na wahadhiri wa uhandisi kwenye nchi kama Urussi,

Ulaya ya Mashariki , Korea Kusini, Japani na kwingineko ambao wangelipenda

sana kuja kukutana na changamoto zetu za kuwa taifa linaloweza kutengeneza

matrekta madogo kwa makubwa yake lenywe; baiskeli zake lenyewe; pikipiki lake

lenyewe; magari yake lenyewe; reli na treni zake lenyewe; meli na feri zake;

maturbine yake ya gesi na maji lenyewe; barabara zake lenyewe; viwanja vya

ndege vyake lenyewe; bandari zake lenyewe za baharini au ziwani au nchi kavu;

pampu zake kubwa kwa ndogo za maji lenyewe; mitambo na mashine kwa

viwanda vyake vidogo lenyewe na kadhalika.

Ni muhimu suala hili lijitokeze sana katika Uandikaji wa Katiba mpya ili kujenga

baada ya hapo mazingira mapya yatakayokuwa mazingira rafiki na azizi katika

kufanikisha ndoto hizo hapo juu.

Na hili haliwezekani bila wahandisi wetu wa leo kuja kuzungumza na kuandaa

mazingira ambayo wahandisi wa kesho watajiona ni zawadi kwa taifa na sio mzigo

usio na faida. Ushiriki wa wahandisi katika baraza au mkutano wa kitaifa wa katiba

kwa hivyo ni kitu adhimu na kinachohitajika sana.

Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie

kwake au sio?



Makampuni yetu ya maji, umeme, viwanda na miradi mingine kama hiyo haitafufuka na kuendelea bila kuwashirikisha Wahandisi na kuwaachia kuwa viongozi wa sekta hiyo. Siasa zinaharibu zaidi maendeleo ya viwanda na siasa hazifai katika sekta ya viwanda.



HakiKatiba DEMOKRASIA ya kweli huheshimu mgawanyo wa madaraka na kazi. Wanasiasa wanaojitia ni mabingwa na maprofesa wa kila kitu hawatatufikisha mbali.

8. MWANDISHI WA HABARI.

HAPA tuwalenge waandishi wa habari ambao ama wanatumiwa na serikali katika

vyombo vya serikali ambavyo vilistahili kuwa vya umma na wale wanaotumiwa na

wanasiasa katika vyama vya upinzani.

Cha kushangaza ni kuwa serikali na chama tawala vimekuwa vinatumia wakati

wake mkubwa kuonya kuwepo kwa udini nchini lakini vinashindwa 'kuaddress'

hasa kinachoweza kuwa chanzo kikubwa cha udini nchini nacho ni vyombo vya

habari na waandishi wa habari kama tulivyoona Rwanda, C'ote d'Ivoire na

kwingineko Afrika.

Tunapozungumzia TBC au Daily News au Habari Leo ni lazima vyombo hivi vya

habari kwanza, kabla ya yote, viwe ni vya umma na sio vya serikali. Hili likifanyika

Wakurugenzi na Wahariri wa vyombo hivyo hawatatishwa au kutumiwa au

kutumika na viongozi wa serikali na chama tawala kwa maslahi yao. Vyombo hivyo

vitakuwa huru na ambavyo vitafanya kazi bila kumuonea au kumpendelea mtu au

chama au upande wowote kutokana na shinikizo za ndnai na nje ya chombo

husika.

Na sisi waandishi wa habari tunahitaji kujipanga na kukataa kutumika kama

changudoa kutokana na ule ukweli wenye kututumia wana ajenda zao. Na ajenda

hizo zinaweza kuishia kutupeleka na sisi kwenye Mahakama za Taifa kama

waangamizaji watu na nchi zetu. Tuwe makini.

Kwa hiyo ni muhimu sana kuwepo na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba

Mpya 2011 ili sisi waandishi wa habari tuwasilishe barazani humo jinsi

tunavyoamini nchi iendeshwe ili vyombo vya habari kama ilivyo Marekani au

Uingereza kweuli uwe ni mhimili wa nne wa kutegemea katika jengo la ghorofa

ndefu la demokrasia na haki ya binadamu tuliloanza kulijenga kimashamashaka

ifanyike kwa ari kuu, wito na dhati ya moyo na matendo.


Demokrasia yetu, penda tusipende haitajengwa na polisi wanaowapiga na kuwanyanyasa raia bali na Vyombo vya Habari Vinavyosema Ukweli!
HakiKatiba

8. MWANDISHI WA HABARI.

HAPA tuwalenge waandishi wa habari ambao ama wanatumiwa na serikali katika

vyombo vya serikali ambavyo vilistahili kuwa vya umma na wale wanaotumiwa na

wanasiasa katika vyama vya upinzani.

Cha kushangaza ni kuwa serikali na chama tawala vimekuwa vinatumia wakati

wake mkubwa kuonya kuwepo kwa udini nchini lakini vinashindwa 'kuaddress'

hasa kinachoweza kuwa chanzo kikubwa cha udini nchini nacho ni vyombo vya

habari na waandishi wa habari kama tulivyoona Rwanda, C'ote d'Ivoire na

kwingineko Afrika.

Tunapozungumzia TBC au Daily News au Habari Leo ni lazima vyombo hivi vya

habari kwanza, kabla ya yote, viwe ni vya umma na sio vya serikali. Hili likifanyika

Wakurugenzi na Wahariri wa vyombo hivyo hawatatishwa au kutumiwa au

kutumika na viongozi wa serikali na chama tawala kwa maslahi yao. Vyombo hivyo

vitakuwa huru na ambavyo vitafanya kazi bila kumuonea au kumpendelea mtu au

chama au upande wowote kutokana na shinikizo za ndnai na nje ya chombo

husika.

Na sisi waandishi wa habari tunahitaji kujipanga na kukataa kutumika kama

changudoa kutokana na ule ukweli wenye kututumia wana ajenda zao. Na ajenda

hizo zinaweza kuishia kutupeleka na sisi kwenye Mahakama za Taifa kama

waangamizaji watu na nchi zetu. Tuwe makini.

Kwa hiyo ni muhimu sana kuwepo na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba

Mpya 2011 ili sisi waandishi wa habari tuwasilishe barazani humo jinsi

tunavyoamini nchi iendeshwe ili vyombo vya habari kama ilivyo Marekani au

Uingereza kweuli uwe ni mhimili wa nne wa kutegemea katika jengo la ghorofa

ndefu la demokrasia na haki ya binadamu tuliloanza kulijenga kimashamashaka

ifanyike kwa ari kuu, wito na dhati ya moyo na matendo.


HakiKatiba HATUTAWEZA kuvifufua na kuviendesha viwanda vya mafanikio bila mchango wa Wahandisi wetu wenyewe!

9. OFISA MISITU

WEWE ofisa misitu wilayani Kisarawe ambaye serikali toka ikupeleke huko

imekusahau kabisa na ofisi yenu ina fenicha za mwaka 1940 na kijumba chenyewe

kinatishia kusambaratika wakati wowote hivi unadhani kweli usipowakilishwa na

wewe mwyewe au mtu anayefanya kazi kama yako mawazo na mchango wa

kuboresha maisha yako leo na kesho itapatikana na itatendewa haki katika

mchakato wa Katiba mpya.


Haiwezekani. Amka. Zinduka na dai haki yako ya kuwa

na Mwakilishi wako katika Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya na

usikubali kabisa kuwakilishwa na wasiojua wapi kunguni na chawa

wanaokusumbua walipo.


Kwa upande mwingine ni wajibu wa wakuu wako wa kazi kama kweli wanataka

kuhakikisha kwamba wewe si mwizi wa mali asili ya nchi hii na haushirikiani na

majangili na wavunaji misitu isivyo halali ni lazima wahakikishe unapewa fursa ya

kuwakilishwa ili uifanye kazi yako kizalendo nawe upate mahitaji yako ya msingi na

ziada kutokana na kazi yako bila kuvunja sheria

za nchi.


HakiKatiba: Mchango wa Mabwana na mabibi Misitu ni Muhimu sana. Nao wawepo kwenye Baraza la Katiba Mpya 2011 ili wizi na uharamia kwa misitu na mali asili ya nchi hii vikome!

10. BWANA, BIBI KILIMO.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?




Wakubwa wamekutekeleza, wamekupuuza, wamekudharau na wamekusahau kwa

miaka yote hii na sasa wao wenyewe ndio wanaojifanya wataalamu zaidi yenu

katika masuala ya kilimo na kufanya maamuzi juu ya vichwa vyenu. Je, unadhani

kilio chako na matarajio yako yatafikishwa na nani kama pasipokuwepo na Baraza

au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 ?

11. MENEJA, MKURUGENZI MTANZANA
RAIS wenu mmoja toka chama tawala aliwatoa manani kabisa na kusema

hamuwezi chochote na wala siyo nyie mtakaoijenga Tanzania bali wawekezaji na

mameneja kutoka nje.

Huu ni wakati muafaka wa kutokosa nafasi yenu ya uwakilishi katika Baraza au

Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 ili muweze kujibu mapigo hayo baada ya

kujipanga kwa hoja na vifungu vitakavyoingia hatimaye kwenye katiba ya nchi hii.

Binafsi sioni sababu ya nyie kwa elimu na ujuzi wenu:
i. Kukosa kutambulika, heshima na tunzo za juu za kitaifa;
ii. Kulipwa mishahara mizuri kuliko Mameneja wageni (walioulia mbali

mashirika ya umma na yale yaliyobinasishwa) na Wanasiasa wa nchi hii na

kwanini wanasiasa hao hususan wabunge wasilipwe kutokana na elimu na ujuzi

wao tu;
iii. Mdai uhuru wa kuendesha mashirika na makampuni kama watu uhuru

bila kuyumbishwa na wanasiasa daima;
iv. Kuweza kufikia kilele cha mafanikio yenu kupitia kazi yenu ikiwemo

katika kipato, elimu, ujuzi na mchango wenu kwa taifa bila kulazimika kuwa

wanasiasa;
v. Kukubalika kwa nafasi yenu iwe mmo katika mashirika ya umma au

mashirika binafsi kama viongozi wa Kiuchumi katika nchi yetu.


HakiKatiba 2011

12. MWANAFUNZI.



MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?


WANAFUNZI wa Kitanzania tokea chekechea wana haki kadhaa wanazozikosa nazo zinatambulika na kila mmoja wetu lakini ni kazi yao kuuelezea umma juu ya shida, dhiki, upungugu, dharau, unyanyasaji, kupuuzwa kwao na kutoshirikishwa kwao katika maamuzi na shughuli mbalimbali za kishule na jinsi ambavyo yote haya yakisahhishwa shule na vyuo nchini mwetu patakuwa ni eneo la utulivu, utafiti, ushauri, elimu na maarfia mapya wakati wote.

Kwanza, majengo na samani katika madarasa kwenye shule nyingi ni jambo linalostahili fungu maalum la bajeti kila mwaka kwa kuzingatia uchakavu na uharibifu wa vitu unaotokea kila mwaka kama sio kila mwezi.


WATANZANIA tuna kila sababu ya kuikataa tabia inayojitokeza na kujijenga Afrika ya kuwatumia polisi na wanajeshi wetu kuwapiga, kuwatia ulemavu au hata kuwaua baba zao, mama zao, ndugu zao, kaka zao, dada zao, watoto wao, rafiki na jamaa zao. Na hili linataka demokrasia kamili, pana, refu na ya kina lakini wakati huo huo ikikataa usiri, uozo, uongo, ulaghai na kuwadanganya wananchi na rushwa, wizi na ufisadi unaolindwa na kuenziwa na chama cha kiasiasa ili kiendelee kubaki madarakani milele.



HakiKatiba 2011

13. MTUMISHI WA UMMA.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Wewe kama mtumishi wa umma na ili mradi unatimiza wajibu wako huna sababu

kabisa ya wewe kuhusishwa na siasa kama hutaki. Vyama vinatakiwa vije

madarakani na kuondoka bila ya wewe kupoteza au kukosa chochote au kudhurika

kwa njia moja au nyingine, wewe na familia yako. Tazama kwa wenzetu

Ujerumani, Uingereza, Ufarsana na Mareknai mambo yanavyofanyika namna hii.

Mnakumbuka baadhi yenu mliokuwa wanafunzi wangu miaka ya kati ya muongo

huu na jinsi ambavyo Waziri Mkuu fulani alivyokuwa akiruhusu wawekezaji kuja

kwako moja kwa moja ili uwafanyie shotikati na jinsi wanavyotaka wao na sio

sheria na kanuni zinavyotaka na mkaja kunilalamikia, wengine mkilia kwamba

mmetukana ?

Hili ndio tatizo la kuwa na Katiba ambayo inaruhusu wapita njia, yaani, wanasiasa

wa vyama fulani kuathiri maisha ya watumishi wa kudumu mawizarani, mikoani na

wilayani. Serikali lazima iwe serikali kweli na haiwezekani na haikubaliki kabisa

kwa chama chochote cha kisiasa katika demokrasia ya kweli kuingilia kazi za

mtumshi wa umma.

14. MZAWA WA MKOA FULANI.

WEWE mkazi wa mkoa fulani hivi unadhani mkoa wako utaendelezwa kwa

kutegemea viongozi, rais, mawaziri,wabunge na watumishi wa umma wanaoishi na

kula upepo wa bahari ya Hindi jijini Dar es salaam au unahitaji sana serikali

iliyokuwa karibu na wewe katika kufanikisha maendeleo yote ya mkoa ikiwemo

yale ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni, kimichezo, kiteknolojia na kimaisha

kwa ujumla.

Mimi ninaamini ewe Mtanzania mwenzangu uliyeko Arusha, Mwanza, Mara,

Mbeya, Kilimanjaro, Ruvuma, Kagera na mikoa iliyosalia kwamba wakati umefika

wa kuondokana na viongozi wanaotembelea mikoa yetu mara moja kwa mwaka

kama sio kila baada ya miaka 5 kunpokuwa na uchaguzi. Na tunahitaji viongozi

ambao ukiamka asubuhi unaweza kusema leo naenda kwa Waziri Mkuu au waziri

wangu kwenda kumwambia anifanyie hiki maana huyu ni mtumishi wangu, mimi ni

mwajiri na yeye ni mfanykazi wangu. Kinyume cha unavyokwenda kwa Mkuu wa

Mkoa au Mkuu wa Wilaya ukitetemeka na ukiamini kwamba yeye ni Bwana

Mkubwa, Tajiri, Bosi wako wakati mambo yanatakiwa yawe kinyume cha hivyo.

Njia ya kufanikisha hili, ndugu yangu Mtanzania, ni kuendelea kuwa na serikali ya

Muungano wa Tanzania na Mikoa yetu ambayo mingi ni mikubwa kieneo na kwa

idadi ya watu kuliko Zanzibar yenye watu milioni moja tu -kuwa na Serikali huru

kiuchumi na kijami za mkoa.

Serikali ya Mkoa itakuwa chini ya Waziri Mkuu wa MKoa (kama ilivyo Ujerumani au

India); chini ya Waziri Mkuu kutakuwa na Baraza la Mawaziri wa Mkoa

watakaotokana na wawakilishi wa wananchi watakaochaguliwa kutoka maeneo

mbalimbali lakini pia watakaotokana na makundi ya kimaslahi katika mkoa husika.

Tofauti na serikali kuu mawaziri wa mkoa watakaotokana na ubunge

wakishachagulwa kuwa mawaziri wataachia nafasi zao za ubunge kwa watu

wengine, ili wabunge wafanye kazi moja tu nayo ni ya kuwakilisha wakazi wa

maeneo au makundi maslahi yao.

Hii ina maana CHADEMA au CUF au NCCR huko tunakokwenda inaweza ikawa

na Waziri Mkuu wa Mkoa na wawakilishi/wabunge wengi kutoka chama hicho na

hivyo kuunda srikali yao. Kwa maneno mengine, CCM inaweza ikawa imeshika

uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini mkoa wa Kilimanjaro au

Mara ukawa chini ya serikali ya CHADEMA na hivyo kuleta chachu kali na

ushindani mkali wa kuuendeleza mkoa na watu wake kuliko nchi nzima inapokuwa

chini ya chama kimoja tu cha kisiasa.

Hili hakika ni jambo zuri na la kupigiwa debe. Na ni wewe mkazi wa mkoa husika

unayeweza kuleta mapinduzi haya makubwa ya kimuundo na kimfumo wa serikali,

jambo litakalochangia kuwepo kikweli kweli kwa ari, kasi na nguvu mpya katika

mandeleo ya nchi na mikoa yake shirikishi kuliko ilivyokuwa huko nyuma.

15. HAKIMU, JAJI



MAJAJI na MAHAKIMU mmeona hoja za Tundu Lissu zilizokuwa kwa yakini na

mashiko yote ya kisheria na haki kwa upande wenu yalivyopinduliwa katika

chombo kilichostahili kuwakilisha maslahi yenu. Kisha wakakubali eti wanasiasa

ndio wawe mabwana nidhamu wenu. Kwa mtaji huu hivi mnaamini kwamba kuna

mtu atakayewakilisha maslahi na kilio chenu cha miaka mingi kwa ukamilifu na

kuwatendea haki kama mwakilishi huyo siye mtu atakayetoka miongoni mwenu. Hii

sio sababu tosha ya nyie pia kudai kuwepo kwa Baraza la Katiba Mpya 2011 ?




Bila shaka Majaji, mahakimu na wanasheria wetu wameona 'laivu' jinsi ambavyo bunge letu linaweza kukabiliana na hoja za msingi zenye mantiki, ukweli na maana isiyokanushika wala kukatalika lakini bado bunge likakataa hoja hiyo au hoja hizo na kuamua tofauti na matarajio ya wengi.

Uweledi, ushujaa na uzalendo wa mbunge mpya na machachari Tundu Lissu ni ushahidi wa hili. Ingawa yeye ni mbunge aliamua kuona ukweli wa kuwa na mihimili ya kitaifa yenye nguvu na haki sawa bila upande mmoja kuudhulumu mwingine au kuunyima haki yake.

Ukweli huu haukuonekana na wabunge wa chama tawala ambao ghafla walipofuka macho na kushindwa kuona kutokana na uchama, umimi na ukabila wao wa kichama.

Hii ni nafasi yenu ya kipekee majaji, mahakimu na wanasheria au wanataaluma katika sheria kuona kuwa haki inatendeka siku zijazo kwa misaada ambayo nguvu ya hoja inaifanya istahili kushinda na sio kushindwa na hoja za mabavu, uchama na uwezo au maamuzi-kabla ya chama kinachotawala.

WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

WATANZANIA tuna kila sababu ya kuikataa tabia inayojitokeza na kujijenga Afrika ya kuwatumia polisi na wanajeshi wetu kuwapiga, kuwatia ulemavu au hata kuwaua baba zao, mama zao, ndugu zao, kaka zao, dada zao, watoto wao, rafiki na jamaa zao. Na hili linataka demokrasia kamili, pana, refu na ya kina lakini wakati huo huo ikikataa usiri, uozo, uongo, ulaghai na kuwadanganya wananchi na rushwa, wizi na ufisadi unaolindwa na kuenziwa na chama cha kiasiasa ili kiendelee kubaki madarakani milele.

16. MWANASIASA, MBUNGE.

WANASIASA wote mnastahili kuwa na mwakilishi kutoka chama chenu kwenye

Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na sio vinginevyo. Maana nyie

ndio vinara wenyewe na washughulikia siasa wakuu na wasimamizi wakuu

baadaye wa haki za raia wote.

Kila chama kina mipango, mikakati,sera na mbinu za kuendeleza jamii ya

Kitanzania. Mathalani, kuna wanaopinga kuwepo kwa serikali huru za mikoa kwa

madai kwamba kufanya hivyo kutavunja umoja na amani yetu. Wakati wengine

wanaunga mikono mikoa kuwa na waziri mkuu wake, mawaziri wa mkoa na

wawakilishi wa mkoa kama vile ile inayoittwa nchi ambayo ni ndogo kwa eneo na

idadi ya watu kuliko mikoa mingi Tanzania ilivyo iitwayo Zanzibar.

Isitoshe wanasiasa wanatofautiana katika masuala ya Muungano, mbinu bora za

kubinafsisha au kutaifisha tena mashirika, viwanda na vyote vilivyoshindwa

kufanya kazi hadi wa leo, Haki za binadamu, elimu bure au elimu kulipiwa na

wazazi au walezi, mikakati sahihi ya kuipatia nchi maji dhidi ya mikakati mibovu,

uhuru wa mtu na uhuru wa vyama na vikundi vya watu,Uwekezaji, uzawa,

Uchimbaji madini na mrabaha, kasi ya kuleta demokraasia,nafasi ya mabenki na

taasisi za fedha katika jamii, kuwepo au kutokuwepo mashirika au makampuni ya

umma, umilikaji na uendeshwaji wa vyombo vya habari vya serikali na kadhalika.

Yote haya yanahitaji mawazo tofauti na mchakato

Kuwepo kwao katika Baraza la Katiba Mpya Tanzania 2011 kutachangia sio haba

kupata katiba bora zaidi na mwelekeo mpya wa kisera, kimpango na kimkakati

katika miaka ijayo ili kuwa na Tanzania madhubuti, bora, safi na tajri kuliko hii ya

sasa. Inshallah!


WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

WATANZANIA tuna kila sababu ya kuikataa tabia inayojitokeza na kujijenga Afrika ya kuwatumia polisi na wanajeshi wetu kuwapiga, kuwatia ulemavu au hata kuwaua baba zao, mama zao, ndugu zao, kaka zao, dada zao, watoto wao, rafiki na jamaa zao. Na hili linataka demokrasia kamili, pana, refu na ya kina lakini wakati huo huo ikikataa usiri, uozo, uongo, ulaghai na kuwadanganya wananchi na rushwa, wizi na ufisadi unaolindwa na kuenziwa na chama cha kiasiasa ili kiendelee kubaki madarakani milele.

17. MWANAKIJIJI.

WANAKIJJI ni watu waliosahaulika sana. Kilichoonekana muhimu kwao na

pengine wamekipata hadi wa leo lakini kwa baadhiya wanavijiji tu ni zahanati,

shule na matawi ya vyama vya siasa vilivyo hoi bin taabani.

Upo umuhimu wa Hazina kuchangia kuwa na matawi imara na madhubuti ya

vyama vyote vya siasa katika kila kijiji na mipango ikafanyika ya kuwawezesha

viongozi wote wa vyama vya kisiasa kuajiriwa kwa njia moja au nyingine na

kulipwa na vyama vyao kutokana na mapato yao na misaada toka Hazina na

wafadhili wanaosaidia harakati halali za kidemokrasia zisizo na nia ya kuichafua

nchi.

Kodi ya wananchi inapotumika kuviendesha vyama vya siasa sio kitu kibaya kwa

maana ufadhili wa nje ni hatari zaidi. Na fedha hizi ni MTAJI WA KIJAMII halisi

ambao unaweza ukawa na thamani kubwa kuliko hata mtaji wa kifedha katika

maendeleo yetu.

Demokrasia na haki za binadamu zikishashamiri vijijini itakuwa ni rahsi wanavijiji

sasa kudai maji ya bomba wakapata; kudai umeme wakapata; kudai barabara safi

na ikawepo; kutafuta masoko ya mazao yao ndani na nje na wao wenyewe

wakauza wanacholima na kuvuna bila kupitia mkononi mwa walanguzi na wakorofi

wengine.

Ni kwa namna hii huduma zilizopo kama vile zahanati, shule, ujenzi wa nyumba za

kisasa vijijini, maoko, bustani za kupumzika, viwanja vya michezo, mawasiliano,

usafi na utunzaji mazingira navyo vitaboreshwa na kusasaishwa zaidi.

WANAVIJIJI walio na uchungu na maendeleo ya vijiji vyao ndio wanaotakiwa

kuleta katika Baraza au mkutano wa katiba mpya ruia na matarajio haya ili

yafaniwe kazi katika katiba na iwe ni kosa kukubali wanavijiji kukosa maji, umeme,

barabara na huduma zingine za msingi na za ngazi ya juu zinazohitajiwa nao.

18. POLISI, WANAJESHI.

KAMA sehemu muhimu ya Ulinzi na Usalama wa nchi ni lazima kuwe na

wawakilishi wa uhakika na watakaochangia juu ya fikra na mtazamo mpya kuwa

nini iwe ni nafasi ya majeshi yetu ya ulinzi na usalama baada-Katiba mpya.

Kuna maswali kadhaa yakujiuliza:

i. Turuhusu kama nchi nyingine za kishenzi zinavyofanya kuwasakazia

raia polisi na jeshi. Na kisha kuwatia ulemavu, kuwajeruhi na hata kuwaua na

hivyo kusababisha wake kukosa waume na watoto kukosa baba na mama. Kiasi

kwamba tunamfanya Mtanzania mmoja akubali kuelekeza mtutu wa bunduki na

kufyatua risasi dhidi ya baba yake, mama yake, mwanawe au mjukuu wake?

ii. Kwanini Mkuu wa Polisi asiteuliwe na kuwa mtii kwa Bunge tukufu la

nchi yetu baada-Katiba ?

iii. Kwanini majeshi yasiape kuwa watii na waaminifu kwa WANANCHI WA

TANZANIA na siyo rais tu. Na katika kuchagua wapi pa kuegemea sikuzote

wachague wananchi na sio viongozi walioko madarakani ?

iv. Tuzuie vipi rushwa ya kifedha, kicheo, kisiasa na nyinginezo katika

majeshi yetu ?
v. Kwa kuzingatia kujitoa mhanga kwa polisi na wanajeshi wetu ni

mshahara gani unaostahili kuwa kima cha chini kwa jeshi ili wasishawishike na

rushwa za aina zote?

vi. Je, polisi na jeshi tukiacha siasa za Uswahilini waishi katika jamii au

wawe na makambi maalum?

vii. Nni nafasi ya majeshi na polisi wetu katika kuhakikisha amani na

usalama kwa kuchangia amani na usalama wa nchi jirani?

viii. Nini kiwe kiwango cha chini cha elimu kwa askari polisi na wanajeshi

katika karne hii ya sayansi na teknolojia?

ix. Je, Polisi jamii kweli wanahitajika au huku ni kukoroga mambo

kutokana na kuishiwa kimawazo kwa viongozi wetu na kwamba katika nchi hii

pawe na specialization na sio kila 'jack and jill' aweze kuwa askari?

x. Je, wakati wa amani na salama nchini majeshi yetu kwanini yasiingie

katika shughuli za uzalishaji mali na kuisadia jamii kupata mahitaji yake ya msingi

haraka zaidi badala ya sisi kuishi kama vile Mtanzania wa leo ataishi milele?

xi. Nini kifanyike ili polisi, jeshi na wanausalama wetu wasitumiwe hata

kidogo na vyama vya siasa na wanasiasa wetu na kutuvuruga Watanzania na

nchi yetu ?


WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

WATANZANIA tuna kila sababu ya kuikataa tabia inayojitokeza na kujijenga Afrika ya kuwatumia polisi na wanajeshi wetu kuwapiga, kuwatia ulemavu au hata kuwaua baba zao, mama zao, ndugu zao, kaka zao, dada zao, watoto wao, rafiki na jamaa zao. Na hili linataka demokrasia kamili, pana, refu na ya kina lakini wakati huo huo ikikataa usiri, uozo, uongo, ulaghai na kuwadanganya wananchi na rushwa, wizi na ufisadi unaolindwa na kuenziwa na chama cha kiasiasa ili kiendelee kubaki madarakani milele.

19. MBUNGE, MWANASIASA.

BILA kufungwafungwa na ubinafsi, umimi na uchama tujiulize maswali haya:

i. Nini nafasi ya mbunge katika nchi inayotaka kujenga demokrasia na

kudumisha haki za binadamu (tofauti na maneno ya kiongozi wa chama fulani

anayedai eti mfumo wa vyama vingi uliletwa na IMF na sio Watanzania.) na kulea

kukuza hulka ya ushindani na maisha ndani ya jamii inayokubali tofauti zake lakini

ikaishi kwa kushirikiana katika kujenga taifa bora na madhubuti zaidi kiuchumi,

kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiteknolojia?

ii. Je, wakati haujafika wa kuwa na Tume huru ya uchaguzi hata kabla ya

mchakato wa Katiba Mpya haujaanza?

iii. Je, kisheria na kikatiba hatuoni 'tumejikwaa' tunapokataa kuwepo kwa

Mgombea huru nchini kwetu.

iv. Je, baadhi ya kanuni na misingi ya kukubaliana ndani ya chama hata

kama kuna makosa makubwa yanatendeka haijapitwa na wakati. Na sio vyema

kuruhusu waziwazi migogoro ndani ya chama ili kukisaida chama kuwa bora zaidi.

v. Nini uwe uhusiano wa rais na serikali kwa upande mmoja na wabunge,

watumishi wa umma na wanasiasa kwa upande mwingine.

vi. Nini kiwe kiwango cha chini cha elimu ya mwanasiasa ili viongozi wa

chini wawe na elimu, uwezo na maarifa ya kuongoza vyema kuliko ilivyo hivi sasa

?

vii. Nini kifanyike ili wabunge wasiwe mateka wa serikali na vyama vya

kisiasa katika kufanya maamuzi yao ? Kwa maneno mengine wabunge wasiwe

wanalindwa na serikali au chama cha siasa bali walindwe na nguvu na heshima ya

bunge la Jamhuri ya Tanzania na ikiwezekana kuwe na bunge la pili kudhibiti

shughuli kwa kiasi fulani kati ya wabunge hawa na serikali yao na mkuu wa nchi?

viii. Kwanini tusiwe na Chuo Kikuu kinachofundisha kwa Kiswahili ili angalau

madiwani wetu, wenyeviti serikali za mitaa, makatibu kata na viongozi katika

matawi ya vyama huko chini wapate digrii ya kwanza, ya pili na ya tatu kwa

kiswahili katik masuala ya uchumi, menejimenti na uongozI?

ix. Je, wakati haujafika kwa wabunge na wanasiasa kuangalia uwezekano

wa kuwa na serikali huru kiuchumi na kijamii kimkoa ili kuufikisha uongozi karibu

zaidi na wananchi kuliko ilivyo sasa. Serikali huru kiuchumi na kijamii za mikoa

zitakazoruhusu kuwepo kwa Waziri Mkuu, mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa

bunge la mkoa ambao kazi yao kubwa ni kuhakikisha kwamba maendeleo ya

kiuchumi na kijamii katika mkoa hayavurugwi na serikali kuu. Aidha, rasilimali na

mali asili za kila mkoa kutumika kwanza kwa manufaa ya wakazi wa mkoa husika

tofauti na ilivyo sasa. Serikali ambazo pia zitaweza kupata ushirikiano na misaada

toka nje moja kwa moja?

x. Je, hakuna umuhimu wa kuwepo na chombo huru nje ya serikali na

vyama vya kisiasa ili kuhakikisha kuwa katiba na sheria za nchi zinafanya kazi na


WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.


wanaokosea kukosolewa na kuchukuliwa hatua zifaazo?

20. BAHARIA NA MARUBANI

NCHI YETU imepoteza ajira nyingi kwa mabaharia, wafanyakazi wa relwe na

wafanyakazi katika ndege na viwanja vya ndege kutokana na viongozi wetu

kushindwa kuhakikisha kuwa mashirika husika yanaendeshwa kwa ufanisi na

ufanifu.

Je, kuna yeyote yule atakayewasilisha mawazo, fikra, imani na matarajio yenu

kuhusu vyombo hivi ila nyie wenyewe au wawakilishi wenu katika mkutano au

baraza la kuandika katiba mpya?

Tukiacha ujinga na upumbavu wa kujitanya tunajua kila kitu na kuwachagua

mameneja wa mashirika nyeti kama wale wa mashirika ya ndege, relwe, meli na

vyombo vingine vya usafiri na tukautanguliza Utanzaznia badala ya ujuzi, uzoefu,

utaalamu na uwezo wa mtu kuongoza iwe Mtanzania au isiwe Mtanzania hatutafika

mbali.

Haya mambo ya nchi nzima kutawaliwa na wafuasi wa chama kimoja tu ndiyo

yametufikisha hapa tulipo leo. Maana ni wanachama hao hao waliokuwa pia

wasimamizi wa mashirika mengi yaliyokufa.

Isitoshe Watanzania wengi wenye uwezo, akili, busara, hekima, ujuzi ulio na soko

na vipaji maalum sio wote wako kwenye chama tawala. Kusimamia uchumi sio

sawa na kusimamia siasa. Katika kusimamia uchumi ni lazima tuachane kabisa ya

kuchagua viongozi kwa sababu ni wananchama na sio kwa sababu wana uwezo

wa kuendesha kitu fulani.

Hasara tunayoipata ndiyo hii ya nchi yetu kukosa shirika la ndege kwa kuwa

mamaneja walikuwa wanachama wa chama fulani. Na mashirika ya relwe ndioi

kama vile hayapo na huko kwenye bahari na kwenye maziwa Tanzania na

Watanzania hawana hata chombo kimoja cha maana cha kujivunia kama watu na

nchi.

Wewe nahodha, baharia au mfanyakazi melini au kwenye ndege unaamini hivi

kweli kuna mtu anayeweza kuwakilisha kilio chako na matarajio yako isipokuwa

mwakailishi wako ambaye atayachukua na kuyapeleka kwenye Baraza la Katiba

Mpya Tanzania 2011 yote yaliyo akilini mwako ili yasikilizwe na kuzingatiwaa

katika kuandika Katiba Mpya ?

21. Mtafiti

PAMOJA na kutambua umuMWANAMICHEZOhimu wa Vyuo Vikuu na vyuo

vingine bado Tanzana iko nyuma sana katika kuwawezesha watafiti kuendesha

tafiti mbalimbali zitakazoweza kuboresha maisha ya Mtanzania.

Utafiti na Uendelezaji vitu na taasisi ni kitu muhimu sana katika jamii. Kutokana na

hili inafaa serikali yoyote kujipanga kwa namna ambayo saa zote walimu,

wahadhiri na maprofesa wa vyuo na vyuo vikuu wanakuwa wana utafiti au ushauri

fulani wanaotekeleza ili kutatua tatizo fulani lililopo au kuwafungua watu na serikali

macho kuhusu fursa zinazojitokeza na jinsi zinavyoweza kutumika ili kuinufaisha

nchi.

Sio hivyo tu, nchi hii na viongozi wamekithiri kwa kuwa wachache wa shukrani na

hasa pale wanapotumia mawazo au fikra za mtu fulani kutangaza, kufanya au

kuamua jambo fulani. Na hili linafanywa na watu wa chini mpaka viongozi wa juu.

KUna uwizi wa aina nyingi, lakini ni vyema pia kujua unaweza ukawa mwizi wa

mawazo ya mtu mwingine. Huu hauna tofauti na wizi mwingine na dhambi ya wizi

wa aina zote haitofautiani kwa maoni yangu. Kweli mtu anaweza asilipe fedha au

kumshukuru mhusika moja kwa moja, lakini ni uungawana na ustaarabu kwenye

hotuba au maandishi iwe kitabu au gazeti ijulikane ni wapi umelipata wazo hilo na

kwamba wewe siye mwasisi wake bali yupo mtu mwingine.

Ni dhahiri, tabia hii kadri inavyoendelea inaondoa kabisa imani na kuaminana kati

ya watu. Na funga na kufumbua utakuta tuna nchi ya matapeli na watu wa kuibiana

sio tu mawazo, bali hata vitu vingine pia na bado mtu akaona hajafanya kosa na eti

kafanya kitu cha halali kabisa.

Yapo mengi yanayowakatisha tamaa watafiti. Ipo mifano ya watafuta PhD.

wanaolipwa milioni 3 kwa miaka yote ya masomo, wakati wenzao hata nchi jirani

wanalipwa milioni 26 kwenda juu. Aidha, uwezo wa kununua vitabu na majarida ni

chini, uwezo wa kununua kompyuta nao nadra, maktaba zetu zimechoka,

upatikanaji data shida tupu, usafiri mashaka, mawasiliano mzigo na kadhalika.

Watafiti lazima wawepo katika Baraza la Katiba Mpya 2011, ili wahakikishe

kwamba kile wanachotaka kukifanyia Watanzania na nchi yao, nahitaji yao,

matarajio yao viwe ni vitu vinavyoeleweka na kuwekwa ipasavyo ndani ya Katiba

mpya,


WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

22. Mwanasayansi

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Ni jukumu la serikali kuwa na mipango, mikakati na sera sahihi zinazohakikisha

kwamba taasisi, zana na vifaa vyote unavyohitaji wewe kama mwanasayansi japo

sio vya kutufikisha mwezini vinakuwepo.

Ni jambo la kutia aibu kwamba katika miaka hii tuna shule za sekondari na vyuo

ambavyo havina hata maabara ya kemia, bayalojia, fizikia na uhandisi wa kemikali

na mambo kama hayo.

Mwanasayansi wetu ambaye mara nyingi ni mtafiti pia ni rasilimali adimu.

Tukiacha kuwapatia vitu wanavyohitaji ili kufanya kazi zao inakuwa ni rahisi sio

wao kukimbia bali serikali na wansiasa wetu kuwafukuza wakaenda kuishi na

kufanya kazi nchi za nje tena kwa maslahi bora zaidi mara 10 ya yale ya hapa

nyumbani.

Huruma kwa watu wao na uzalendo wao, hata hivyo, tukiacha kuwafanyia kile

wanachokitrajia huishia tu pale maslahi ya watoto na familia zao yanapokosekana.

Hakuna mtu mwingine anayeweza kuwasaidia ili Katiba iainishe sio tu wajibu wao

kwa jamii bali pia haki na kuhitajika kwao na nchi na watu wake kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

23. Diwani

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Kwa kuwa maendeleo hayatoki juu bali yanatokea chini kwa wananchi. Na diwani,

wajumbe wa nyumba kumi, makatibu kata na viongozi wa serikali za mitaa ni watu

muhimu sana katika uongozi huu wa ngazi za chini, je, kuna mipango yoyote ya

kuhakikisha kwamba watu hawa, yaani, wewe diwani na wenzako mnapatiwa

elimu itakayowasaidia kufaulisha kazi zenu ?

Ni kichekesho katika dunia ya leo kuwa na diwani ambaye hajasomea lolote

kuhusu uchumi, menejimenti, biashara, nadharia za kodi, menejimenti ya muda,

saikolojia, sosholojia, menejimenti ya fedha, masoko au nunuauza, uzalishaji mali,

ujasriamali, misingi ya uhasibu, menejmenti ya rasilimali watu na mengineyo kama

hayo.

Na hili linatokea pamoja na jitihada za wanaharakati wa maumizi ya Kiswahili

kupondwa na viongozi wa awamu mbalimbali wa nchi hii.

Lakini kama tungelikuwa tunatoa elimu kwa lugha ya Kiswahili toka ngazi ya shule

za msingi hadi Chuo au Chuo Kikuu angalau kwa viongozi wa serikali za mitaa,

mashule na taasisi za umma basi viongozi wetu wangeliweza kuhitimu vyema tu

katika masomo hayo na kuitumikia watu na nchi yao kwa ufanisi na ufanifu wa hali

ya juu zaidi.

UTAFITI UNAONESHA KWAMBA ASILIMIA 94 YA WATANZANIA HAWAJAWAHI

KATIKA MAISHA YAO KUKUTANA NA MWINGEREZA, MFARANSA, MRENO,

MHISIPANIA, MCHINA, MJAPANI na kuzungumza naye kwa lugha nyingine

yoyote isipokuwa KISWAHILI.

Ni asilimia hiyo 94 ya Watanzania inayotuhoji pia kwanini tunakataa kuwafundisha

elimu na maarifa mapya kwa lugha mama yao Kiswahili.

Je, wakati haujafika wa kuwa na Taasisi iwe binafsi au ya umma ambayo itakuwa

ikitoa elimu ya chekechea, msingi, sekondari, chuo hadi chuo kikuu kwa kiswahili

katika masomo yote kama taasisi ya mfano na majaribio ili kutathmini kwa vitendo

na kufanya maamuzi sahihi kuhusu nafasi ya Kiswahili Tanzania, Afrika Mashariki

na duniani kwa ujumla ?

Diwani unawajibika kuingia katika Baraza la Katiba mpya ili kusaidia kuwa na

katiba ambayo pamoja na kushinikiza matumizi mapana na marefu ya Kiswahili

itachangia Watanzania wengi zaidi kuelimika na kuneemeka na lugha mama yao.

WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

24. Mbunifu, Mvumbuzi

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Hivi inawezekana sisi Watanzania tu wazito na wavivu kiasi cha kukosa hata

asilimia chache tu ya watu wetu wenye uwezo wa kuwa wabunifu na wavumbuzi

wa vitu, maarifa, mifumo na miundo mipya ya uendeshaji mambo ili kusaidia

kuharakisha maendeleo ya watu na nchi yetu ?

La, hasha. Soma magazeti na tazama televisheni utaona kuna wabunifu na

wavumbuzi wengi tu wa mambo mbalimbali. Ni serikali na wanasiasa ndio

walioshindwa kuandaa taasisi zenye mipango, mikakati, sera, muundo, mifumo

na watu wanaoweza kuchochea moto wa ubunifu na uvumbuzi badala ya kuuzima.

Wabunifu na wavumbuzi wote undeni kikundi cha dharura ili kuchagua watu wa

kuwasilisha madai, kilio na matakwa yenu mnayotaka yaangazwe katika katiba

mpya. Wakati ni huu, chelewa chelewa utamkuta mtoto si wako!

25. Msanii, Mwanamuziki.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Tanzania ina kila sababu ya kuongoza Afrika katika muziki, ngoma, filamu, redio,

telelvisheni, magazeti, michezo ya kuigiza na maeneo yote ya sanaa na muziki

endapo tu viongozi wetu watakuwa mstari wa mbele kwenda kufanya kazi kule

wananchi waliko na sio kujifungia kwneye maofisi yao yenye viyoyozi kule Dar es

salaam.

Tunapozungumzia mafanikio ya sekta hii hakika tunazungumzia mabilioni ya

shilingi yatakayotiririka kwenye hazina ya taifa na kuipunguzia nchi umaskini, elimu

duni na tiba zisizoridhisha za afya. Aanayechezea namna hii shilingi chuoni hivi

anafaa kuwa kiongozi wa Watanzania?

Ni lazima tuoneshe njia kwa kushiriki katika Baraza la Katiba Mpya ili serikali iwayo

ijue tunataka sekta yetu ya muziki na usanii iendeshwe vipi na sio kwa huruma na

msaada wa huyu au yule ambaye hatakuwa nasi au na kizazi chetu kijacho daima.

26. Mvuvi

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Tanzania bado ina uvuvi wa enzi za Sultan Barghash. Ipo haja ya wavuvi kuja na

hoja ya kuitaka serikali kutoka na mipango, mkakati, sera na mwongozo wa Uvuvi

Kwanza kwa niaba ya wakazi wa maeneo karibu na maziwa na bahari. Mkakati

utakaowawezesha wavuvi kuanzisha vikundi vya kijamii (CBOs) au ushirika

kuufanya uvuvi kuwa wa kisasa na wenye tija na faida kwao.

Na wavuvi hawawezi kufanikiwa katika hili bila kilio na matarajio yao kufikishwa

kwenye Baraza la Katiba Mpya 2011 na matakwa yao kuzungumziwa kwa ufupi

ndani ya katiba na kirefu katika sheria, miipango na sera zitakazotengenezwa

baada ya kutoka kwa Katiba Mpya.

27. Mfugaji, Mrinaasali

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

TANZANIA ina kiola sababu ya kuwa muuza nyama, maziwa na asali mkubwa

Afrika ya Mashariki na Kati. Lakini hili linataka mipango mizuri, mikakati, sera na

utekelezaji unaowashirikisha wadau wote kwa kuunganisha masoko ya nje na

wazalishaji hapa nyumbani.

Kunahitajika ushirikiano na watafiti, washauri wa ujasirimali, uzalishaji mali,

menejimenti na masoko ili kifanyike kinachohitajika kufanyika kwa manufa ya

wafugaji wanyama, nyuki, mamba, ndege na hata nyoka kwa faida ya wafugaji hao

na taifa lao kiujumla.

28. Dereva, Konda

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Dereva na konda mnatukanwa na wenye mabasi, hamna ajira, mnatukanwa na

trafiki na wanafunzi na mnadhulumiwa na wenye vituo vya mafuta na kadhalika.

Yote haya ni mambo ambayo kama nchi ingelikuwa na sera, taratibu na kanuni

sahihi za uendeshaji mambo yasingewapa shida kwa kiasi cha shida mnazopata

leo. Mna kila haki ya kuwasilisha maoni yenu hadi ngazi ya juu kabisa ya tamko la

taifa kuipitia mchango wenu kwenye Baraza la Katiba Mpya 2011.

Udereva sio kazi ndogo. Ungelikuwa kazi ndogo pasingekuwa na madereva

wanaolipwa 250,000/-500,000- kwa mwezi kwa kuendesha wakubwa. Au hamjui?

Mna kila sababu ya kudai ajira za kudumu, kutetea maslahi na marupurupu yenu

na usalama wenu kazini na wakati ni huu kuotkana na fursa inayoletwa na

mchakato wa Katiba mpya nchini. Ila ni lazima muwe na mwakilishi wenu msije

kuwakilishwa na waajiri wenu!

29. Mkopaji.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Inavyoelekea hivi leo Benki, Vyama vya Kuweka na Kukopa, taasisi za

Microfinacne na wakopeshaji wa aina zote wananufaika zaidi ya Mtanzania

anavyonufaika na kuna madai ya taasisi hizo kuwanyonya watu.

Je, ili sisi kama wakopaji wa Kitanzania tunahitaji Taasisi gani za fedha ? Na nini

iwe mchango wa Benki Kuu, NSSF, PPF, LAPF, NHSF na wengine kama hao?

Na, je, makampuni ya simu ambayo sasa yanatukopesha kisirisiri na kucheza

kamari zinazotula kila siku hazivuni kupita kiasi. Je, mashirika kama haya ya simu

hayastahili kuwekea sheria ya kuuza sehemu zao za hisa kwa wananchi ili

kugawana na Watanzania mabilioni yote wanayoyafaidi kila mwezi ?

30. Mkopeshaji.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako, matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na yanayokugusa?

Ni lazima mkopeshaji naye alindwe na kupata haki zake. Lakini hilo linakuwa rahisi kama mkopeshaji huyo anawatendea haki wale anaowakaposha, yaani, wakopaji.

Kukopa na kukopesha ni kitu kizuri katika jamii kama kinafanya kazi iliyokusudiwa nayo si ya kamari bali ya kinyenzo kama msaada unaokuja usipotegemewa kumuondoa mtu katika hali duni na dhaifu na kumpeleka katika hali bora. Ikiwa ni kinyume cha hivyo basi huitwa mtego na umumiani wa kiuchumi ambao unakuwa hauna faida kwa mwananchi.

Mkopeshaji lazima afikirie sikuzote kuwa tofauti na wenzake na katika kuwa tofauti huku ni lazima Benki Kuu na serikali vimzawadiwe kwa njia moja au nyingine. Kwa mfano, kuzuka kwa benki ambazo wafanyakazi wengi watakuwa mitaani kukutana na watu mbalimbali wakiwemo wazalishaji mali, wakulima, wafanyabiashara na wajasiriamli wengine kwa nia ya kuwashauri na kuwaendeleza katika shughuli zao kama Benki za Wajapani zinavyofanya kuanzia mwaka 1955 itakuwa na uwezo wa kufanya maajabu kuliko benki nyingine nchini.

Na hili haliwezekani bila wakopeshaji wenyewe kuwa na ubia na wakopaji katika shughuli zao kwa faida ya pande zote.

31. MTOTO WA KIJIWENI.

NDUGU yangu unaona nuru au mwanga katika maisha yako. Nani anajua unavyoshinda na njaa; unavyotaka kuelimika lakini hakuna wa kukuelimisha; unavyotaka kuoa lakini uwezo huna; unavyotaka kuchukua nafasi yako katika kuchangia maendeleo ya nchi yako lakini hauna fursa.

Je, hivi kuna mtu anaweza kukuwakilisha wewe, mawazo na fikra zako na kadhalika ili viwemo ndani ya Katiba mpya. Kwanini usiwe na mwakilishi wako katika mkutano au baraza la katiba mpya?

Hvi upo hapo kijiweni kwa sababu ya kupenda au kwa kuwa umekosa mtu wa kuendeleza kipaji chako au kukusomesha au kukupatia ajira.

Unafikiri hawa wanasiasa wanaokupa samaki badala ya kukupa nyavu za kwenda kuvua wewe mwenyewe wanakusaidia?

Isingelikuwa vizuri uwepo wako hapa duniani uwe na sababu nawe uwe unaifuata sababu hiyo. Au inatosha tu kupewa ruksa na chama fulani kwamba hapa wekeni kijiwe chenu nasi tutawalinda. Na sio hawa hawa wanasiasa watakaowazuza hapo baadaye mwende pambana na vijana wenzenu toka vyama vingine mambo yatakapowaharibikia kama kilichotokea kwa Gbagbo na mwenzake Outtara ? Wao wako haki na wanafaidi maisha na walichokwiba na kupata kwa halali vijana wengi wameuawa, wamekuwa vilema na wengine wanateswa na kuozea kwenye magereza. Hii siyo njia ya kuchagua kwa kweli. Chagua kushiriki katika Baraza

la Katiba Mpya Tanzania ili uweze kufikisha unachotaka kuwa ili usije kutumika kama chakula cha risasi huko twendako.

32. KIJANA, MSICHANA, MVULANA.

UNGELIPENDA kuwa na nchi ya aina gani unapokuja kuwa mtu mzima. Je, kuna mtu yeyote anayeweza kukusemea fikra, ndoto, maoni, matarajio na matazamio yako. Unahitaji uwakilishi wa vijana wenzako au wazee na wasomi waliosahau ujana na maisha ya kijana na hofu na

matarajio yake yakoje?

Asilimia hamsini au zaidi ya Watanzania leo ama ni watoto au vijana. Na idadi hiyo inazidikukua siku hadi siku. Katika maendeleo ya nchi yoyote duniani wakati hufika ambapo idadi ya vijana huwa kubwa zaidi kuliko watoto au wazee katika nchi. Kwa kuwa vijana ndio wenye akili angavu zaidi na uwezo zaidi kiaakili na kifikra huu huwa ni wakati muhimu wa kujenga nchi na kuitoa kwenye ngazi ya chini na kuipeleka ya juu au za juu zaidi. Lakini hili hutegemea ni aina

gani ya uongozi uliopo madarakani.

Uongozi ukiwa ni ule wa kuwadanganya wananchi wa samaki wa kila siku badala ya kuwawezesha vijana kwenda kuvua wao wenyewe huishia kuingia kwenye matatizo.

Yanayotokea Misri na nchi za Maghreb na kwingineko Uarabuni ni nchi kuwa na vijana wengi lakini ikashindwa kuwashughulisha vijana hao.Na kama biblia inavyosema nadhani katika Mitahali, mikono isiyokuwa na kazi ya maana ya kufanya basi shetani huwa hachelewi kuitumia.

Je, ni nani atakayewanusuru vijana wa nchi hii na majaliwa hayo kama sio wao wenyewe au wawakilishi wao katika Baraza la Katiba la Kitaifa Tanzania 2011 ?

33. MWANAMKE.

Ewe mwanamke wa Kitanzania ungelipenda kuendelea kuwa mpiga vigelegele, mhudumu na mshangiliaji na mpigaji makofi kwa wanaume au unadhani wakati wa mabadiliko umefika. Hebu jiulize maswali haya:

i. Nini kifanyike ili yanayotokea Uarabuni,Sudan, Kongo na Burundi yasitokee Tanzania ?

ii. Hivi mnastahili kuwa na UMOJA WA WANAWAKE WA TANZANIA (TANZANIA) au Umoja wa Wanawake Tanzania (CCM) ?

iii. Hivi kweli mnahitaji viti na vyeo vya kupewa au mnahitaji mipango na mikakati ya kutumia akili, nguvu na uwezo wenu wenyewe kujiendeleza?

iv. Tuwaangalie vipi wagonjwa wanawake na wajane nchini mwetu?

v. Tumkomboe vipi mwanamke wa vijijini?

vi. Tumewezeshe vipi mwanamke wa Kitanzania ili asibebwe bebwe kila saa?

vii. Tumpe vipi mwanamke wa Kitanzania Uhuru wa kuabudu kwa mujibu wa dini yake ikiwemo pia kuwa na Mahakama ya Kadhi kwa faida ya Wanawake wa Kiislamu na jamaa/jamii yao?

viii. Wanawake wanawezaje kuishinikiza serikali na wanasiasa ili nchi iwe na demokrasia ya kweli na uheshimuji haki za binadamu kwa mapana na marefu? Tukizingatia kwamba wanaoteseka na kuaibika kunapokoseakana demokrasia ya kweli zaidi ni wanawake?

34. MWANAMICHEZO, FIZIKALI.

NCHI yenu imedorora kupitta kiasi katika michezo na baadhi yenu sasa mmeanza kutumika kama punda wa kubeba madawa ya kulevya, je, nini kifanyike kuinusuru michezo na sanaa katika nchi hii?

i. Michezo mashuleni iboreshwaje ili kuhakikisha kuna kuna shule zinazospeshalaizi katika michezo angalau kila kata kwa msingi na sekondari ili kuandaa maprofeshenoo wa siku zijazo, walimu wa michezo, viwanja vya michezo, mashindano wakati muafaka, lishe bora, usafiri salama na malezi na ulinzi muafaka wa wanamichezo makambini?

ii. Je, tutegemee mtu mmoja kuendeleza michezo au kuwe na taasisi, sera tumikifu, mifumo inayofanya kazi, bajeti/fedha, viongozi bora na safi na misaada ya hali na mali toka serikalini, mikoani na wilayani. Aidha, matumizi bainifu na ya wazi ya misaada toka ndani na nje ya nchi toka mashirika na watu binafsi?

iii. Kwanini michezo na sanaa zisiwekwe chini ya Mamlaka zinazojitgemea, yaani, zisiwe ni sehemu ya wizara bali ni taasisi huru zinazowezeshwa na kulindwa na serikali na lengo la kuja kujiendesha zenyewe kutokana na mapato yake ya ndani na nje ya nchi kutokana na ushiriki wake katika mashindano na shughuli mbalimbali? Kwa mfano, biashara kuuza wachezaji soka nchi za nje isipoangaliwa inaweza kuwa ni uuzaji watu na ikaja wanufaisha watu wachache tu na sio nchi nzima kwa ujumla?

iv. Tufufuaje michezo iliyokufa au yenye hatari ya kufa kama vile riadha, ngumi, mbio za magari, mbio za pikipiki, mbio za baiskeli na mengineyo kama hayo?

v. Tuwekeje uwazi katika malipo au fedha anazopata mchezaji ili wasiendee kudhulumiwa na viongozi wa michezo, mapromota, wauzaji wanamichezo na wasanii, makocha na walimu wa michezo na sanaa ? Na hatimaye wanamichezo na wasanii wapate mapato ya kuridhisha yatakayowachochea kufanya vizuri zaidi na kuwavuta wengine kwenye michezo na sanaa?

Je, mwanamichezo na msanii kuna mtu atakayewakilisha kikamilifu ndoto yenu hii na kutetea maslahi yenu kikatiba kama siyo nyie wenyewe kwa kuhakikisha sheria mama, yaani, katiba, inaweka wazi juu ya masuala yote muhimu yanyohusu michezo na sanaa na jinsi gani wanamichezo na wasanii wanavyoweza KUJIAJIRI NA KUTAJIRIKA kutokana na vipawa au vipaji vyao?

Tunapozungumzia mafanikio ya sekta hii hakika tunazungumzia mabilioni ya shilingi yatakayotiririka kwenye hazina ya taifa na kuipunguzia nchi umaskini, elimu duni na tiba zisizoridhisha za afya. Aanayechezea namna hii shilingi chuoni hivi anafaa kuwa kiongozi wa Watanzania?

Ni lazima tuoneshe njia kwa kushiriki katika Baraza la Katiba Mpya ili serikali iwayo ijue tunataka sekta yetu ya muziki na usanii iendeshwe vipi na sio kwa huruma na msaada wa huyu au yule ambaye hatakuwa nasi au na kizazi chetu kijacho daima.