Friday, May 27, 2011

22. Mwanasayansi

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Ni jukumu la serikali kuwa na mipango, mikakati na sera sahihi zinazohakikisha

kwamba taasisi, zana na vifaa vyote unavyohitaji wewe kama mwanasayansi japo

sio vya kutufikisha mwezini vinakuwepo.

Ni jambo la kutia aibu kwamba katika miaka hii tuna shule za sekondari na vyuo

ambavyo havina hata maabara ya kemia, bayalojia, fizikia na uhandisi wa kemikali

na mambo kama hayo.

Mwanasayansi wetu ambaye mara nyingi ni mtafiti pia ni rasilimali adimu.

Tukiacha kuwapatia vitu wanavyohitaji ili kufanya kazi zao inakuwa ni rahisi sio

wao kukimbia bali serikali na wansiasa wetu kuwafukuza wakaenda kuishi na

kufanya kazi nchi za nje tena kwa maslahi bora zaidi mara 10 ya yale ya hapa

nyumbani.

Huruma kwa watu wao na uzalendo wao, hata hivyo, tukiacha kuwafanyia kile

wanachokitrajia huishia tu pale maslahi ya watoto na familia zao yanapokosekana.

Hakuna mtu mwingine anayeweza kuwasaidia ili Katiba iainishe sio tu wajibu wao

kwa jamii bali pia haki na kuhitajika kwao na nchi na watu wake kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.

NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.

Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.

No comments:

Post a Comment