Friday, May 27, 2011

27. Mfugaji, Mrinaasali

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

TANZANIA ina kiola sababu ya kuwa muuza nyama, maziwa na asali mkubwa

Afrika ya Mashariki na Kati. Lakini hili linataka mipango mizuri, mikakati, sera na

utekelezaji unaowashirikisha wadau wote kwa kuunganisha masoko ya nje na

wazalishaji hapa nyumbani.

Kunahitajika ushirikiano na watafiti, washauri wa ujasirimali, uzalishaji mali,

menejimenti na masoko ili kifanyike kinachohitajika kufanyika kwa manufa ya

wafugaji wanyama, nyuki, mamba, ndege na hata nyoka kwa faida ya wafugaji hao

na taifa lao kiujumla.

No comments:

Post a Comment