Friday, May 27, 2011

24. Mbunifu, Mvumbuzi

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Hivi inawezekana sisi Watanzania tu wazito na wavivu kiasi cha kukosa hata

asilimia chache tu ya watu wetu wenye uwezo wa kuwa wabunifu na wavumbuzi

wa vitu, maarifa, mifumo na miundo mipya ya uendeshaji mambo ili kusaidia

kuharakisha maendeleo ya watu na nchi yetu ?

La, hasha. Soma magazeti na tazama televisheni utaona kuna wabunifu na

wavumbuzi wengi tu wa mambo mbalimbali. Ni serikali na wanasiasa ndio

walioshindwa kuandaa taasisi zenye mipango, mikakati, sera, muundo, mifumo

na watu wanaoweza kuchochea moto wa ubunifu na uvumbuzi badala ya kuuzima.

Wabunifu na wavumbuzi wote undeni kikundi cha dharura ili kuchagua watu wa

kuwasilisha madai, kilio na matakwa yenu mnayotaka yaangazwe katika katiba

mpya. Wakati ni huu, chelewa chelewa utamkuta mtoto si wako!

No comments:

Post a Comment