MANESI wetu wanalaumiwa hivi leo kwa kila jambo lakini ukangalia kwa undani ni
suala la mishahara tu na maslahi.
Kwa mtu anayefanya kazi wakati mwingine masaa 10 au zaidi kwa siku,
anayekosa usingizi mara kwa mara na anayetakiwa kutoa huduma ambazo wengi
wetu tutafikiri mara mbili kukubali kuzifanya wakati umefika kwa kweli kuangalia
uwezekano wa kuwa na kima cha chini cha mshahara ambacho kitawavutia
wanawake na wanaume wenye wito kufanya kazi hii ya unesi kwa huruma,
mapenzi na uvumilivu.
Je, wewe nesi unadhani kuna mtu anaweza kuwakilisha kilio, mahitaji, matakwa na
matarajioa yako ila nesi mwenzako uliyemchagua kwenda kusema unachokittaka
kiwekwe hadharani?
Zingatia kuwa serikali na wananchi wa Tanzania wana uwezo wa kuzifanya
hospitali zetu kuwa bora kiasi ambacho wagonjwa wengi katika nchi mbalimbali za
Kiafrika wakaja hapa kutibiwa na kuuguzwa badala ya kupelekwa nchi za nje ? Na
hili likifanyika ni kwamba mishahara, marupurupu yenu na kipato chenu kwa
ujumla kitaongezeka na hamtakuwa na sababu ya kukimbilia nchi za nje !
Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa
na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au
Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,
wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi
kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie
kwake au sio?
NCHI inayowaheshimu madaktari na manesi wake na kuwa na mazingira mazuri kwa wafanyakazi na wagonjwa mahospitalini inaweza kupata fedha za kigeni kutokana na kuja kwa wagonjwa wengi kutoka nchi jirani na za mbali kutibiwa hapa kwetu.
HakiKatiba 2011: Hospitali zetu zikiwa nzuri, daktari na manesi wetu wakaridhika tunaweza kupata mabilioni ya fedha za kigeni!
No comments:
Post a Comment