Friday, May 27, 2011

17. MWANAKIJIJI.

WANAKIJJI ni watu waliosahaulika sana. Kilichoonekana muhimu kwao na

pengine wamekipata hadi wa leo lakini kwa baadhiya wanavijiji tu ni zahanati,

shule na matawi ya vyama vya siasa vilivyo hoi bin taabani.

Upo umuhimu wa Hazina kuchangia kuwa na matawi imara na madhubuti ya

vyama vyote vya siasa katika kila kijiji na mipango ikafanyika ya kuwawezesha

viongozi wote wa vyama vya kisiasa kuajiriwa kwa njia moja au nyingine na

kulipwa na vyama vyao kutokana na mapato yao na misaada toka Hazina na

wafadhili wanaosaidia harakati halali za kidemokrasia zisizo na nia ya kuichafua

nchi.

Kodi ya wananchi inapotumika kuviendesha vyama vya siasa sio kitu kibaya kwa

maana ufadhili wa nje ni hatari zaidi. Na fedha hizi ni MTAJI WA KIJAMII halisi

ambao unaweza ukawa na thamani kubwa kuliko hata mtaji wa kifedha katika

maendeleo yetu.

Demokrasia na haki za binadamu zikishashamiri vijijini itakuwa ni rahsi wanavijiji

sasa kudai maji ya bomba wakapata; kudai umeme wakapata; kudai barabara safi

na ikawepo; kutafuta masoko ya mazao yao ndani na nje na wao wenyewe

wakauza wanacholima na kuvuna bila kupitia mkononi mwa walanguzi na wakorofi

wengine.

Ni kwa namna hii huduma zilizopo kama vile zahanati, shule, ujenzi wa nyumba za

kisasa vijijini, maoko, bustani za kupumzika, viwanja vya michezo, mawasiliano,

usafi na utunzaji mazingira navyo vitaboreshwa na kusasaishwa zaidi.

WANAVIJIJI walio na uchungu na maendeleo ya vijiji vyao ndio wanaotakiwa

kuleta katika Baraza au mkutano wa katiba mpya ruia na matarajio haya ili

yafaniwe kazi katika katiba na iwe ni kosa kukubali wanavijiji kukosa maji, umeme,

barabara na huduma zingine za msingi na za ngazi ya juu zinazohitajiwa nao.

No comments:

Post a Comment