Friday, May 27, 2011

7. MHANDISI.

MIAKA kadhaa Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa Afrika

kuwa na Kitivo cha Uhandisi kwenye Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Vyuo kadhaa vya ufundi ukiachilia mbali vile vya VETA vilivyokuja baadaye pia

vilianzishwa kwa madhumuni kama hayo.

Katikati hapa sera na mwelekeo wa kisiasa umeua au kulemaza sana taasisi zote

ikiwmo viwanda, maabara, vyombo vya usafirishaji na uchukuzi kiasi ambacho

mustakabali wa wahandisi na mafundi wengine uko mashakani.

La kusikitisha ni kuwa Mhandisi wa Kitanzania hadi wa leo hajaweza kutengeneza

hata sindano achilia mbali pasi, balbu, pampu ya maji, baiskeli, redio, televisheni

achilia mbali mashine na mitambo inayotakikana kwa uzalishaji hili au lile.

Serikali hii imebweteka mno kuhusu suala la uhandisi na nafas yake katika kutumia

kwa vitendo sayansi, teknolojia na teknohama katika miaka hii ambayo kuna

wahandisi tele na maprofesa na wahadhiri wa uhandisi kwenye nchi kama Urussi,

Ulaya ya Mashariki , Korea Kusini, Japani na kwingineko ambao wangelipenda

sana kuja kukutana na changamoto zetu za kuwa taifa linaloweza kutengeneza

matrekta madogo kwa makubwa yake lenywe; baiskeli zake lenyewe; pikipiki lake

lenyewe; magari yake lenyewe; reli na treni zake lenyewe; meli na feri zake;

maturbine yake ya gesi na maji lenyewe; barabara zake lenyewe; viwanja vya

ndege vyake lenyewe; bandari zake lenyewe za baharini au ziwani au nchi kavu;

pampu zake kubwa kwa ndogo za maji lenyewe; mitambo na mashine kwa

viwanda vyake vidogo lenyewe na kadhalika.

Ni muhimu suala hili lijitokeze sana katika Uandikaji wa Katiba mpya ili kujenga

baada ya hapo mazingira mapya yatakayokuwa mazingira rafiki na azizi katika

kufanikisha ndoto hizo hapo juu.

Na hili haliwezekani bila wahandisi wetu wa leo kuja kuzungumza na kuandaa

mazingira ambayo wahandisi wa kesho watajiona ni zawadi kwa taifa na sio mzigo

usio na faida. Ushiriki wa wahandisi katika baraza au mkutano wa kitaifa wa katiba

kwa hivyo ni kitu adhimu na kinachohitajika sana.

Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima avutie

kwake au sio?



Makampuni yetu ya maji, umeme, viwanda na miradi mingine kama hiyo haitafufuka na kuendelea bila kuwashirikisha Wahandisi na kuwaachia kuwa viongozi wa sekta hiyo. Siasa zinaharibu zaidi maendeleo ya viwanda na siasa hazifai katika sekta ya viwanda.



HakiKatiba DEMOKRASIA ya kweli huheshimu mgawanyo wa madaraka na kazi. Wanasiasa wanaojitia ni mabingwa na maprofesa wa kila kitu hawatatufikisha mbali.

No comments:

Post a Comment