Friday, May 27, 2011

10. BWANA, BIBI KILIMO.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?




Wakubwa wamekutekeleza, wamekupuuza, wamekudharau na wamekusahau kwa

miaka yote hii na sasa wao wenyewe ndio wanaojifanya wataalamu zaidi yenu

katika masuala ya kilimo na kufanya maamuzi juu ya vichwa vyenu. Je, unadhani

kilio chako na matarajio yako yatafikishwa na nani kama pasipokuwepo na Baraza

au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 ?

11. MENEJA, MKURUGENZI MTANZANA
RAIS wenu mmoja toka chama tawala aliwatoa manani kabisa na kusema

hamuwezi chochote na wala siyo nyie mtakaoijenga Tanzania bali wawekezaji na

mameneja kutoka nje.

Huu ni wakati muafaka wa kutokosa nafasi yenu ya uwakilishi katika Baraza au

Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 ili muweze kujibu mapigo hayo baada ya

kujipanga kwa hoja na vifungu vitakavyoingia hatimaye kwenye katiba ya nchi hii.

Binafsi sioni sababu ya nyie kwa elimu na ujuzi wenu:
i. Kukosa kutambulika, heshima na tunzo za juu za kitaifa;
ii. Kulipwa mishahara mizuri kuliko Mameneja wageni (walioulia mbali

mashirika ya umma na yale yaliyobinasishwa) na Wanasiasa wa nchi hii na

kwanini wanasiasa hao hususan wabunge wasilipwe kutokana na elimu na ujuzi

wao tu;
iii. Mdai uhuru wa kuendesha mashirika na makampuni kama watu uhuru

bila kuyumbishwa na wanasiasa daima;
iv. Kuweza kufikia kilele cha mafanikio yenu kupitia kazi yenu ikiwemo

katika kipato, elimu, ujuzi na mchango wenu kwa taifa bila kulazimika kuwa

wanasiasa;
v. Kukubalika kwa nafasi yenu iwe mmo katika mashirika ya umma au

mashirika binafsi kama viongozi wa Kiuchumi katika nchi yetu.


HakiKatiba 2011

No comments:

Post a Comment