Friday, May 27, 2011

8. MWANDISHI WA HABARI.

HAPA tuwalenge waandishi wa habari ambao ama wanatumiwa na serikali katika

vyombo vya serikali ambavyo vilistahili kuwa vya umma na wale wanaotumiwa na

wanasiasa katika vyama vya upinzani.

Cha kushangaza ni kuwa serikali na chama tawala vimekuwa vinatumia wakati

wake mkubwa kuonya kuwepo kwa udini nchini lakini vinashindwa 'kuaddress'

hasa kinachoweza kuwa chanzo kikubwa cha udini nchini nacho ni vyombo vya

habari na waandishi wa habari kama tulivyoona Rwanda, C'ote d'Ivoire na

kwingineko Afrika.

Tunapozungumzia TBC au Daily News au Habari Leo ni lazima vyombo hivi vya

habari kwanza, kabla ya yote, viwe ni vya umma na sio vya serikali. Hili likifanyika

Wakurugenzi na Wahariri wa vyombo hivyo hawatatishwa au kutumiwa au

kutumika na viongozi wa serikali na chama tawala kwa maslahi yao. Vyombo hivyo

vitakuwa huru na ambavyo vitafanya kazi bila kumuonea au kumpendelea mtu au

chama au upande wowote kutokana na shinikizo za ndnai na nje ya chombo

husika.

Na sisi waandishi wa habari tunahitaji kujipanga na kukataa kutumika kama

changudoa kutokana na ule ukweli wenye kututumia wana ajenda zao. Na ajenda

hizo zinaweza kuishia kutupeleka na sisi kwenye Mahakama za Taifa kama

waangamizaji watu na nchi zetu. Tuwe makini.

Kwa hiyo ni muhimu sana kuwepo na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba

Mpya 2011 ili sisi waandishi wa habari tuwasilishe barazani humo jinsi

tunavyoamini nchi iendeshwe ili vyombo vya habari kama ilivyo Marekani au

Uingereza kweuli uwe ni mhimili wa nne wa kutegemea katika jengo la ghorofa

ndefu la demokrasia na haki ya binadamu tuliloanza kulijenga kimashamashaka

ifanyike kwa ari kuu, wito na dhati ya moyo na matendo.


HakiKatiba HATUTAWEZA kuvifufua na kuviendesha viwanda vya mafanikio bila mchango wa Wahandisi wetu wenyewe!

No comments:

Post a Comment