Friday, May 27, 2011

5. MWALIMU.


MWALIMU kwenye miaka ya 1960 mara tu baada ya mkoloni kuondoka

walipendwa, kuaminiwa na kuheshimika lakini sio leo.

Je, tuanwezaje kurudisha upendo, imani na heshima kwa walimu hapa Tanzania?

Kilichofanyika hadi kufikia hapa ni kwamba wanasiasa waliamini kwamba wao ndio

wanaostahili kulipwa mishahara mizuri kuliko walimu wetu. Na kwamba ualimu si

kazi ya maana, wanaotaka waingie na wasiotaka watoke kirahisirahisi tu.

Matokeo yake ndiyo hayo ya kuporoka kila siku viwango vya elimu iwe ni msingi,

sekondar au high school!




Usahihishaji mitihani ndao unakuwa wa kibabe, kinuni na unaochangia

wasahihishaji kuondoka na zigo la madhambi kwa sababu ya kukosa kutenda haki

kwa watahiniwa. Hivi leo anayetegemewa kufaulu anaweza akafeli na mtu wa

kufeli akafaulu eti kwa sababu za kiufundi au kiteknohama. Lakini ukweli ni kuwa

upo uwezekano mkubwa wa haki sasa kununuliwa na wengine kudhulumiwa.



Tatizo ni mfumo wa usahihishaji uliopo ambao hauna wakati mwingine 'local

external examiner' na 'external examiner' kutoka nchi za nje ili kukamata uhalifu

huu katika 'sampling' itakayofanyika kiufundi na kijanja.

Lakini pia malipo kwa wasahihishaji yanapokuwa kidogo au wanapokuwa

wanapunjwa na maofisa husika au wanapokosa hazi zao nyingine kama wasahihi

shaji hili ni jambo la kutegemewa.


Lakini kubwa zaidi ni lile la kutaka kuitawala nchi nzima kutoka Dar es salaam.

Ninaamini kwa wingi wa shule tulizonazo leo wakati umefika wa kuwa na Bodi za

Mitihani za Mikoa ambazo zingeliandana uzuri sana na lile wazo la kuwa na

serikali huru kiuchumi na kijamii za mkoa. Mitihani itakaposimamiwa katika ngazi

ya mkoa au kanda kwa kuanzia itarahisisha usahihishaji wake na matumizi ya

wasahihishaji/waangalia mitihani toka mikoa mingine na nchi za nje.

Lingine ni lile la kurudisha MItihani yetu yote katika nchi zetu za Afrika Mashariki

iwe chini ya Bodi moja ya Mitihani ya Afrika mashariki kama ilivyokuwa East

African Cambridge enzi hizo!


Jitayarisheni, jiandaeni na kujihami na nguvu za hoja kuhusu umuhimu wa kuwa

na Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya 2011 na wala sio Tume au

Kikundi cha wateuliwa wachache hata kama ni mawaziri, wabunge, majaji,

wanasheria na engineo kama hao, maana historia inaonesha wote hao hawawezi

kutetea maslahi yako wewe na kwamba mwamba ngoma ngozi lazima av


utie kwake au sio?



HakiKatiba 2011 Nchi isyowathamini na kuwalipa mishahara mizuri maprofesa, wahadhiri na walimu wake na badala yake ikakufuru kuwalipa wabunge, wanasiasa na viongozi wa serikali vizuri kuliko kundi hili na mengine kama haya lisahau kabisa kuondokana na umaskini, ujinga, maradhi na kuwa nyuma kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment