Friday, May 27, 2011

6. MHADHIRI, PROFESA.


UKIKUTANA na maprofesa wetu ambao walikuwa wakimuogopa Mungu na kuishi

kimaskini kwa tumaini kuwa mishahara na pensheni zao zingeliwasaidia uzeeni,

aghalabu utatamani kulia.



NI maprofesa na wahadhiri ambao walimwibia mwajiri wao muda au kutumia utafiti

au ushauri kujitajirisha wao binafsi ndio wenye maisha mazuri.

Ipo haja ya kuangalia upya mishahara ya maprofesa na wahadhiri wa vyuo vikuu ili

tupate kilicho bora kutoka kwa na wanafunzi wao. Hivi leo, kwa kiasi kikubwa ni

kwamba tunajidanganya kwamba tunawalipa na wao wanadanganya wanatimiza

wajibu wao.



Njia mojawapo ya kuongeza mishahara na marupurupu ya wasomi hawa ni

kuhakikisha vyuo vikuu vinakuwa na miradi mizuri na toshelevu na endelevu

itakayoingiza kipato cha ziada kitakachotumiwa kwa maslahi ya walimu na

wafanyakazi wengine wa vyuo vikuu, kwa mfano, katika masuala ya kodi za

nyumba, usafiri na manunuzi ya vitabu na visaidizi vingine vya elimu na kisomo.



Namna nyingine ya kuongeza kipato kwa wafanyakazi wa vyuo vikuu vyetu ni

kuvitengea bajeti tosha ya utafiti kazi ambayo itafanywa na wote, walimu kwa

wanafunzi na mwisho wa siku wote watanufaika na kupunguza sana kilio cha

kipato na maslahi. Hili lal utafiti linaendana na matumizi ya ushauri wa walimu na

maprofesa wa vyuo vikuu badala ya serikali zetu kushauriwa na watoto wa mjini au

watumishi wa umma wakiwemo makatibu wakuu na mawaziri wenyewe kufanya

mipango ya kuwa na washauri wa kupanga toka ndani na nje ya nchi.



Endapo kila Mkoa nchini utakuwa na Chuo Kikuu chake cha umma, mishahara na

maslahi ya maprofesa na wahadhiri yana uwezekano mkubwa zaidi wa kuwa bora

na ya kuridhisha zaidi kwa sababu kwanza watakuwa kwenye mikoa ambayo si

ghali kama Arusha, Mwanza, Dodoma na Dar es salaam.



Sio tu kipato na maslahi ya maprofesa na wahadhiri yataongezeka bali hata

maendeleo ya kielimu, kijamii, kiuchumi, kiutamaduni, kisiasa na kiteknolojia ya

mikoa husika itakwenda kwa kasi zaidi kuliko ilivyo hivi sasa.



Na hili linawezekana kwa kuwatumia maprofesa na walimu waliopo hivi sasa na

kugawanya vitivo au fani za masomo mbalimbali ili Chuo Kikuu kimoja kisiwe na

zaidi ya fani 2-3 tu!



Isitoshe kuna maprofesa na wahadhiri wengi tu wasio na kazi kwenye nchi za

Ulaya Mashariki, Urussi na jamaa zake, Ireland, Spain, Portugal na hata Marekani

kwenyewe.



Yote haya yanaweza tu kufanikiwa ikiwa ni wahadhiri na maprofesa wenyewe ndio

watakaokuwa wawakilishi katika Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya

2011.



HakiKatiba 2011 Nchi isyowathamini na kuwalipa mishahara mizuri maprofesa, wahadhiri na walimu wake na badala yake ikakufuru kuwalipa wabunge, wanasiasa na viongozi wa serikali vizuri kuliko kundi hili na mengine kama haya lisahau kabisa kuondokana na umaskini, ujinga, maradhi na kuwa nyuma kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment