WEWE ofisa misitu wilayani Kisarawe ambaye serikali toka ikupeleke huko
imekusahau kabisa na ofisi yenu ina fenicha za mwaka 1940 na kijumba chenyewe
kinatishia kusambaratika wakati wowote hivi unadhani kweli usipowakilishwa na
wewe mwyewe au mtu anayefanya kazi kama yako mawazo na mchango wa
kuboresha maisha yako leo na kesho itapatikana na itatendewa haki katika
mchakato wa Katiba mpya.
Haiwezekani. Amka. Zinduka na dai haki yako ya kuwa
na Mwakilishi wako katika Baraza au Mkutano wa Kitaifa wa Katiba Mpya na
usikubali kabisa kuwakilishwa na wasiojua wapi kunguni na chawa
wanaokusumbua walipo.
Kwa upande mwingine ni wajibu wa wakuu wako wa kazi kama kweli wanataka
kuhakikisha kwamba wewe si mwizi wa mali asili ya nchi hii na haushirikiani na
majangili na wavunaji misitu isivyo halali ni lazima wahakikishe unapewa fursa ya
kuwakilishwa ili uifanye kazi yako kizalendo nawe upate mahitaji yako ya msingi na
ziada kutokana na kazi yako bila kuvunja sheria
za nchi.
HakiKatiba: Mchango wa Mabwana na mabibi Misitu ni Muhimu sana. Nao wawepo kwenye Baraza la Katiba Mpya 2011 ili wizi na uharamia kwa misitu na mali asili ya nchi hii vikome!
No comments:
Post a Comment