Friday, May 27, 2011

14. MZAWA WA MKOA FULANI.

WEWE mkazi wa mkoa fulani hivi unadhani mkoa wako utaendelezwa kwa

kutegemea viongozi, rais, mawaziri,wabunge na watumishi wa umma wanaoishi na

kula upepo wa bahari ya Hindi jijini Dar es salaam au unahitaji sana serikali

iliyokuwa karibu na wewe katika kufanikisha maendeleo yote ya mkoa ikiwemo

yale ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni, kimichezo, kiteknolojia na kimaisha

kwa ujumla.

Mimi ninaamini ewe Mtanzania mwenzangu uliyeko Arusha, Mwanza, Mara,

Mbeya, Kilimanjaro, Ruvuma, Kagera na mikoa iliyosalia kwamba wakati umefika

wa kuondokana na viongozi wanaotembelea mikoa yetu mara moja kwa mwaka

kama sio kila baada ya miaka 5 kunpokuwa na uchaguzi. Na tunahitaji viongozi

ambao ukiamka asubuhi unaweza kusema leo naenda kwa Waziri Mkuu au waziri

wangu kwenda kumwambia anifanyie hiki maana huyu ni mtumishi wangu, mimi ni

mwajiri na yeye ni mfanykazi wangu. Kinyume cha unavyokwenda kwa Mkuu wa

Mkoa au Mkuu wa Wilaya ukitetemeka na ukiamini kwamba yeye ni Bwana

Mkubwa, Tajiri, Bosi wako wakati mambo yanatakiwa yawe kinyume cha hivyo.

Njia ya kufanikisha hili, ndugu yangu Mtanzania, ni kuendelea kuwa na serikali ya

Muungano wa Tanzania na Mikoa yetu ambayo mingi ni mikubwa kieneo na kwa

idadi ya watu kuliko Zanzibar yenye watu milioni moja tu -kuwa na Serikali huru

kiuchumi na kijami za mkoa.

Serikali ya Mkoa itakuwa chini ya Waziri Mkuu wa MKoa (kama ilivyo Ujerumani au

India); chini ya Waziri Mkuu kutakuwa na Baraza la Mawaziri wa Mkoa

watakaotokana na wawakilishi wa wananchi watakaochaguliwa kutoka maeneo

mbalimbali lakini pia watakaotokana na makundi ya kimaslahi katika mkoa husika.

Tofauti na serikali kuu mawaziri wa mkoa watakaotokana na ubunge

wakishachagulwa kuwa mawaziri wataachia nafasi zao za ubunge kwa watu

wengine, ili wabunge wafanye kazi moja tu nayo ni ya kuwakilisha wakazi wa

maeneo au makundi maslahi yao.

Hii ina maana CHADEMA au CUF au NCCR huko tunakokwenda inaweza ikawa

na Waziri Mkuu wa Mkoa na wawakilishi/wabunge wengi kutoka chama hicho na

hivyo kuunda srikali yao. Kwa maneno mengine, CCM inaweza ikawa imeshika

uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakini mkoa wa Kilimanjaro au

Mara ukawa chini ya serikali ya CHADEMA na hivyo kuleta chachu kali na

ushindani mkali wa kuuendeleza mkoa na watu wake kuliko nchi nzima inapokuwa

chini ya chama kimoja tu cha kisiasa.

Hili hakika ni jambo zuri na la kupigiwa debe. Na ni wewe mkazi wa mkoa husika

unayeweza kuleta mapinduzi haya makubwa ya kimuundo na kimfumo wa serikali,

jambo litakalochangia kuwepo kikweli kweli kwa ari, kasi na nguvu mpya katika

mandeleo ya nchi na mikoa yake shirikishi kuliko ilivyokuwa huko nyuma.

No comments:

Post a Comment