MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa
umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe
kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna
mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,
matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe
mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na
yanayokugusa?
Wewe kama mtumishi wa umma na ili mradi unatimiza wajibu wako huna sababu
kabisa ya wewe kuhusishwa na siasa kama hutaki. Vyama vinatakiwa vije
madarakani na kuondoka bila ya wewe kupoteza au kukosa chochote au kudhurika
kwa njia moja au nyingine, wewe na familia yako. Tazama kwa wenzetu
Ujerumani, Uingereza, Ufarsana na Mareknai mambo yanavyofanyika namna hii.
Mnakumbuka baadhi yenu mliokuwa wanafunzi wangu miaka ya kati ya muongo
huu na jinsi ambavyo Waziri Mkuu fulani alivyokuwa akiruhusu wawekezaji kuja
kwako moja kwa moja ili uwafanyie shotikati na jinsi wanavyotaka wao na sio
sheria na kanuni zinavyotaka na mkaja kunilalamikia, wengine mkilia kwamba
mmetukana ?
Hili ndio tatizo la kuwa na Katiba ambayo inaruhusu wapita njia, yaani, wanasiasa
wa vyama fulani kuathiri maisha ya watumishi wa kudumu mawizarani, mikoani na
wilayani. Serikali lazima iwe serikali kweli na haiwezekani na haikubaliki kabisa
kwa chama chochote cha kisiasa katika demokrasia ya kweli kuingilia kazi za
mtumshi wa umma.
No comments:
Post a Comment