Friday, May 27, 2011

29. Mkopaji.

MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa

umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe

kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna

mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,

matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe

mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na

yanayokugusa?

Inavyoelekea hivi leo Benki, Vyama vya Kuweka na Kukopa, taasisi za

Microfinacne na wakopeshaji wa aina zote wananufaika zaidi ya Mtanzania

anavyonufaika na kuna madai ya taasisi hizo kuwanyonya watu.

Je, ili sisi kama wakopaji wa Kitanzania tunahitaji Taasisi gani za fedha ? Na nini

iwe mchango wa Benki Kuu, NSSF, PPF, LAPF, NHSF na wengine kama hao?

Na, je, makampuni ya simu ambayo sasa yanatukopesha kisirisiri na kucheza

kamari zinazotula kila siku hazivuni kupita kiasi. Je, mashirika kama haya ya simu

hayastahili kuwekea sheria ya kuuza sehemu zao za hisa kwa wananchi ili

kugawana na Watanzania mabilioni yote wanayoyafaidi kila mwezi ?

No comments:

Post a Comment