MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa
umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe
kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna
mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,
matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe
mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na
yanayokugusa?
Tanzania bado ina uvuvi wa enzi za Sultan Barghash. Ipo haja ya wavuvi kuja na
hoja ya kuitaka serikali kutoka na mipango, mkakati, sera na mwongozo wa Uvuvi
Kwanza kwa niaba ya wakazi wa maeneo karibu na maziwa na bahari. Mkakati
utakaowawezesha wavuvi kuanzisha vikundi vya kijamii (CBOs) au ushirika
kuufanya uvuvi kuwa wa kisasa na wenye tija na faida kwao.
Na wavuvi hawawezi kufanikiwa katika hili bila kilio na matarajio yao kufikishwa
kwenye Baraza la Katiba Mpya 2011 na matakwa yao kuzungumziwa kwa ufupi
ndani ya katiba na kirefu katika sheria, miipango na sera zitakazotengenezwa
baada ya kutoka kwa Katiba Mpya.
No comments:
Post a Comment