BILA kufungwafungwa na ubinafsi, umimi na uchama tujiulize maswali haya:
i. Nini nafasi ya mbunge katika nchi inayotaka kujenga demokrasia na
kudumisha haki za binadamu (tofauti na maneno ya kiongozi wa chama fulani
anayedai eti mfumo wa vyama vingi uliletwa na IMF na sio Watanzania.) na kulea
kukuza hulka ya ushindani na maisha ndani ya jamii inayokubali tofauti zake lakini
ikaishi kwa kushirikiana katika kujenga taifa bora na madhubuti zaidi kiuchumi,
kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiteknolojia?
ii. Je, wakati haujafika wa kuwa na Tume huru ya uchaguzi hata kabla ya
mchakato wa Katiba Mpya haujaanza?
iii. Je, kisheria na kikatiba hatuoni 'tumejikwaa' tunapokataa kuwepo kwa
Mgombea huru nchini kwetu.
iv. Je, baadhi ya kanuni na misingi ya kukubaliana ndani ya chama hata
kama kuna makosa makubwa yanatendeka haijapitwa na wakati. Na sio vyema
kuruhusu waziwazi migogoro ndani ya chama ili kukisaida chama kuwa bora zaidi.
v. Nini uwe uhusiano wa rais na serikali kwa upande mmoja na wabunge,
watumishi wa umma na wanasiasa kwa upande mwingine.
vi. Nini kiwe kiwango cha chini cha elimu ya mwanasiasa ili viongozi wa
chini wawe na elimu, uwezo na maarifa ya kuongoza vyema kuliko ilivyo hivi sasa
?
vii. Nini kifanyike ili wabunge wasiwe mateka wa serikali na vyama vya
kisiasa katika kufanya maamuzi yao ? Kwa maneno mengine wabunge wasiwe
wanalindwa na serikali au chama cha siasa bali walindwe na nguvu na heshima ya
bunge la Jamhuri ya Tanzania na ikiwezekana kuwe na bunge la pili kudhibiti
shughuli kwa kiasi fulani kati ya wabunge hawa na serikali yao na mkuu wa nchi?
viii. Kwanini tusiwe na Chuo Kikuu kinachofundisha kwa Kiswahili ili angalau
madiwani wetu, wenyeviti serikali za mitaa, makatibu kata na viongozi katika
matawi ya vyama huko chini wapate digrii ya kwanza, ya pili na ya tatu kwa
kiswahili katik masuala ya uchumi, menejimenti na uongozI?
ix. Je, wakati haujafika kwa wabunge na wanasiasa kuangalia uwezekano
wa kuwa na serikali huru kiuchumi na kijamii kimkoa ili kuufikisha uongozi karibu
zaidi na wananchi kuliko ilivyo sasa. Serikali huru kiuchumi na kijamii za mikoa
zitakazoruhusu kuwepo kwa Waziri Mkuu, mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa
bunge la mkoa ambao kazi yao kubwa ni kuhakikisha kwamba maendeleo ya
kiuchumi na kijamii katika mkoa hayavurugwi na serikali kuu. Aidha, rasilimali na
mali asili za kila mkoa kutumika kwanza kwa manufaa ya wakazi wa mkoa husika
tofauti na ilivyo sasa. Serikali ambazo pia zitaweza kupata ushirikiano na misaada
toka nje moja kwa moja?
x. Je, hakuna umuhimu wa kuwepo na chombo huru nje ya serikali na
vyama vya kisiasa ili kuhakikisha kuwa katiba na sheria za nchi zinafanya kazi na
WATAKAOCHANGIA bila uchama, ukabila, ueneo, udini, ubinafsi na ushawishi wowote toka kundi lolote ndani au nje ya nchi watastahili kupewa tunzo ya juu kabisa ya Kitaifa.
NI haki na wajibu wenu pia kuwaamsha, kuwafundisha na kuwaelekeza wananchi wengine nini wanachopaswa kufanza ili mahitaji yao ya msingi, dhiki, mapungufu kwao, kasoro zilizopo kwenye maeneo na maisha yao, haki na maslahi yao yote yaweze kupatikana kwa kutumia katiba na sheria za nchi na sio vinginevyo.
Ni muhimu pia wananchi kuelewa kwamba serikali ni kitu kinachodumu milele mpaka mwisho wa dunia lakini vyama vya kisiasa ni taasisi za kupita, leo vinaweza kuwepo na kesho visiwepo na vikaja vyama vipya kabisa madarakani.
wanaokosea kukosolewa na kuchukuliwa hatua zifaazo?
No comments:
Post a Comment