MTANZANIA wewe ndiye unayemwajiri rais, mawaziri, wabunge na watumishi wa
umma. Na wewe ndiye mmiliki wa Katiba. Na katiba ni mchakato wa wewe
kuwaambia watawala waliopo na wajao unataka utawaliwe vipi na wao. Je, kuna
mtu mwingine anayeweza kuwasilisha ipasavyo unachokitaka kiwe, matakwa yako,
matarajio yako maslahi yako na ndoto ya Tanzania uitakayo na ile ya wewe
mwenyewe unachotaka kuwa kama sio mwakilishi wako anayeguswa na
yanayokugusa?
Tanzania ina kila sababu ya kuongoza Afrika katika muziki, ngoma, filamu, redio,
telelvisheni, magazeti, michezo ya kuigiza na maeneo yote ya sanaa na muziki
endapo tu viongozi wetu watakuwa mstari wa mbele kwenda kufanya kazi kule
wananchi waliko na sio kujifungia kwneye maofisi yao yenye viyoyozi kule Dar es
salaam.
Tunapozungumzia mafanikio ya sekta hii hakika tunazungumzia mabilioni ya
shilingi yatakayotiririka kwenye hazina ya taifa na kuipunguzia nchi umaskini, elimu
duni na tiba zisizoridhisha za afya. Aanayechezea namna hii shilingi chuoni hivi
anafaa kuwa kiongozi wa Watanzania?
Ni lazima tuoneshe njia kwa kushiriki katika Baraza la Katiba Mpya ili serikali iwayo
ijue tunataka sekta yetu ya muziki na usanii iendeshwe vipi na sio kwa huruma na
msaada wa huyu au yule ambaye hatakuwa nasi au na kizazi chetu kijacho daima.
No comments:
Post a Comment